Habari Zote
Archive for November 2022
KKATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja ambaye
hakufahamika kwa jina Amenusurika na kipigo na wananchi Wenye hasira kali mara
baada ya kufanya Uharibifu kwa kuharibu mashine ya Kusaga mahindi ya
Mjasiliamali mwenzake kutokana na wivu wa kimaendeleo.
Kijana huyo mkazi wa kijiji cha Nyikonga wilayani
Mbogwe Mkoani Geita amenusurika na kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali
mara baada ya kuvamia nyakati za usiku na kuanza kuharibu mashine ya kusaga mahindi
iliyo jirani yake inayotumia mafuta ambapo yeye ameajiriwa katika mashine inayotumia
Umeme.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mwenyekiti wa
serikali ya kijiji hicho Mperwa Sekela amesema kesi hiyo kwa sasa iko
mahakamani huku akitoa wito kwa wananchi
kuachana na vitendo vya kujichulia sheria mkononi.
Kwa upande wake mmiliki wa mashine hiyo iliyoharibiwa
hakuwa tayari kuzungumzia tukio hilo huku mmiliki wa mashine alikokuwa
anafanyia kazi kijana aliefanya uharibifu huo amekiri kutokuwa na ugomvi wowote
na jirani yake huku baadhi ya wananchi wakishangazwa na kitendo alichokifanya
kijana huyo.
Mpaka sasa kijana huyo yuko chini ya uangalizi wa
vyombo vya Dola katika hatua zaidi za
uchunguzi wa Tukio alilofanya.
Hayo yameelezwa na baadhi ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye mtaa huo mkutano uliokua unahusu namna ya kuuthibiti uharifu unao fanyika ndani ya mtaa wao.
Wananchi hao wamesema kuwa kuna umuhimu wa kurejesha ulinzi shirikishi ili kuweza kukabiria na vitendo vya uharifu vinavyo fanyika ndani ya mtaa.
Nae mwenyekiti wa mtaa huo ELIMGABI NJIBA ameagiza kuondolewa kwa vijana moja ya nyumba iliyopo mtaani hapo inayo daiwa kufuga vibaka.
Vitendo vya uwizi na udokozi vimeibuka kwa kasi hivi karibuni ndani ya mtaa huo hali iliyo walazimu viongozi wa mtaa huo kufanya mkutano na kupanga mikakati namna ya kukabiliana na uharifu unaofanyika ndani ya mtaa wao.