Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Search This Blog

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Neema Nanukia Mikoa Na Magharibi

Imeelezwa kuwa kukamilika kwa Daraja la Mto Momba linalounganisha mikoa ya Rukwa na Songwe kutafufua fursa za kiuchumi katika mikoa ya magh...

Imeelezwa kuwa kukamilika kwa Daraja la Mto Momba linalounganisha mikoa ya Rukwa na Songwe kutafufua fursa za kiuchumi katika mikoa ya magharibi na kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) mkoa wa Rukwa Eng. Masuka Mkina (wa tatu kushoto), wakati alipokagua daraja la Kinambo lililopo katika  barabara ya Kasansa-Muze KM 31.90  wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amesema hayo leo alipokagua ujenzi wa daraja hilo na kuwahakikishia wananchi wa Wilaya ya Sumbawanga kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha daraja hilo linakamilika mwezi Agosti mwakani.

Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) mkoa wa Rukwa Eng. Masuka Mkina (wa tatu kushoto), akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa (aliyevaa fulana nyeusi), wakati alipokagua daraja la Kinambo lililopo katika  barabara ya Kasansa-Muze KM 31.90  wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.
“Toeni ushirikiano unaostahili kwa mkandarasi ili Daraja hili la Momba na madaraja madogo saba yanayojengwa katika barabara ya Kasansa-Kilyamatundu yenye urefu wa KM 210.38 yakamilike kwa wakati”, amesema Prof. Mbarawa.
Mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi wa daraja la Kinambo lililopo katika  barabara ya Kasansa-Muze KM 31.90  wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.
Amesisitiza nia ya Serikali ya kujenga barabara ya Kasansa-Kilyamatundu KM 210.38 na Stalike-Kilyamatundu-Mloo KM 500 kwa kiwango cha lami ili kuongeza kasi ya uzalishaji na usambazaji wa mazao ya kilimo na mifugo katika Bonde la Mto Rukwa kwenda maeneo mingine ya nchi.
Muonekano wa mitambo ya kuchimbia nguzo za Daraja la Mto Momba unaounganisha mikoa ya Rukwa na Songwe. 
“Wale wote ambao wamewekewa alama za kubomoa nyumba zao ili kupisha ujenzi wa barabara nawaomba wafanye hivyo mapema ili kuwawezesha wakandarasi kufanya kazi zao kwa uhuru na kuiwezesha TANROADS kufanya usanifu wa kina”, alisisitiza.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya Jiangxi Geo-Engineering (Groups) Corporation, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mto Momba linalounganisha mikoa ya Rukwa na Songwe.
Naye Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) mkoa wa Rukwa Eng. Masuka Mkina, amemhakikishia Prof. Mbarawa kuwa watamsimamia kikamilifu mkandarasi anayejenga Daraja la Momba na madaraja madogo saba katika barabara ya Kasansa-Kilyamatundu KM 210.38 ili kazi ujenzi huo ukamilike kwa wakati.
Mbunge wa Jimbo la Kwela Mhe. Ignas Malocha, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, wakati wa mkutano na wananchi wa Kilymatundu mara baada ya kukagua ujenzi wa Daraja la Mto Momba, wilayani Sumbawanga.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kwela Ignas Malocha, amewataka wananchi watakaopata fursa za ujenzi wa madaraja hayo kuepuka vitendo vya wizi na hujuma kwa wakandarasi.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na wananchi wa Kilymatundu mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mto Momba, wilayani Sumbawanga.
Amesema kukamilika kwa Daraja la Momba kuna manufaa mengi kiuchumi, kijamii kwa kuwa daraja hilo litawaunganisha wakazi wa jimbo lake na mkoa wa Songwe na hivyo kuharakisha shughuli za kimaendeleo.
Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Kilyamatundu kilichopo wilayani Sumbawanga akimkabidhi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, ushahidi wa picha za miti iliyokatwa katika shamba lake kupisha mradi wa ujenzi wa Daraja la Mto Momba, mkoani Rukwa.

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Neema Nanukia Mikoa Na Magharibi
Neema Nanukia Mikoa Na Magharibi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_u6LTwCspstOO3eP4npPGdGN6jZ6F9QIHW22NVrMIUpZ6Z0t85UsVSSMnvschlfVmxsmAYoxH42uFijhtXDl7pvuZw3YF8JG_0jHAMviicehMBjkFpW9HQpZc_hqJK95SZIujcVS-PBs/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_u6LTwCspstOO3eP4npPGdGN6jZ6F9QIHW22NVrMIUpZ6Z0t85UsVSSMnvschlfVmxsmAYoxH42uFijhtXDl7pvuZw3YF8JG_0jHAMviicehMBjkFpW9HQpZc_hqJK95SZIujcVS-PBs/s72-c/1.JPG
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/10/neema-nanukia-mikoa-na-magharibi.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/10/neema-nanukia-mikoa-na-magharibi.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content