Habari Mpya

Thursday, 19 October 2017

UONGOZI wa mkoani Simiyu umembadilishia majukumu  ya kazi Tabibu, Laurent Biyengo na kuwa mlinzi katika lango kuu la kuingilia hospitali kutokana na kushindwa kuyamudu majukumu ya kitabibu.
 
Waziri wa Afya ,Ustawi wa jamii,Wazee,Jinsia na Watoto,Ummy Mwalimu
Biyengo ambaye anadaiwa kushindwa kuingia kazini na kwenda kulewa saa za kazi alipokuwa zamu septemba 27 mwaka huu na kusababisha ujauzito aliokuwa nao Salome John kutoka kwa kushindwa kupatiwa huduma.

Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika kutoka ndani ya hospitali hiyo na kuthibitishwa na baadhi ya matumishi wenzake zinaeleza kuwa tangu aanze majukumu yake hayo mapya sasa ni kipindi cha majuma mawili akilinda getini.

Wakizungumza na hivi karibuni, baadhi ya madaktari hao walisema kuwa adhabu aliyopewa ni ya haki kutokana na kitendo alichokifanya ambacho kinakiuka maadili ya taaluma yao ya utabibu.

“Huyu mwenzetu amepata adhabu ya haki na hii wamemsaidia sana maana alipaswa kufukuzwa kazi haiwezekani umepangwa kutoa huduma za kitabibu katika hospitali kubwa kama hii halafu unakwenda kulewa na kusababisha wagonjwa kutopata huduma, nikukiuka maadili ya kitabibu,”alisema Daktari mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Walisema kuwa kitendo alichokifanya kimewapotezea imani kwa wagonjwa wanaofika kupata matibabu katika hospitali hiyo, huku wengine wakitumia lugha za kuwakejeli na kuwadhihaki jambo ambalo linawashusha molali ya kazi.

Kwa mujibu wa habari za kuaminika kutoka chanzo ambacho kilifika katika hospitali ya wilaya ya Maswa na kumshuhudia daktari huyo akiwa katika lango kuu la kuingilia hospitalini hapo, na kumwona  akufungulia magari na pikipiki zinazoingia na kutoka sambamba na watu wanaokuja kupata matibabu hata hivyo jitihada za kuongea naye hazikuzaa matunda baada ya kugoma kuongea.

Akizungumzia suala hilo Mkuu wa wilaya ya Maswa Dk. Seif Shekalaghe alikiri kwa daktari huyo kubadilishiwa majukumu ya kazi na kusisitiza kuwa hiyo ni hatua ya awali walizozichukua kutokana na kitendo alichokifanya.

“Nimeambiwa ya kuwa amebadilishiwa majukumu ya kazi kutoka kutoa huduma za kitabibu na kuwa mlinzi lakini nahisi kuna hatua zaidi ya hiyo inatakiwa kufanywa nipeni muda tutapata majibu sahihi,”alisema Shekalaghe.


Kufuatia tukio hilo,Waziri wa Afya ,Ustawi wa jamii,Wazee,Jinsia na Watoto,Ummy Mwalimu alimwelekeza Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Dk. Zainab Chaula kumchukulia hatua.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -