Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Makala ya Elimu

KUTOKANA na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kuendelea kutokea katika jamii yetu, katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mashirika na asa...

KUTOKANA na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kuendelea kutokea katika jamii yetu, katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mashirika na asasi mbalimbali, zikiwemo za serikali na binafsi zimekuwa zikiendelea kutoa elimu kwa jamii ili iweze kuachana na vitendo hivyo unavyovota ni vikinyama
 
 Mwanamke mmoja akitoka shambani kulima huku akiwa amebeba mzigo mkubwa wa kuni, mtoto mgongoni na mwingine akiwa amemshikilia mkono. mume wake amemwachia kufanya kazi zote. Huo ni ukatili wa kijinsia
Mbali na kutoa elimu hiyo pia asasi na mashirika hayo yamekuwa yakitumia fursa hiyo kuwakumbusha wanajamii madhara ya ukatili huo, ikiwa ni pamoja na adhabu inayotolewa kwa mtu au kikundi chochote kilichofanya ukatili wa kijinsi dhidhi ya mtu au watu furani.

Lakini pamoja na kutolewa kwa elimu ndani ya jamii yetu baadhi ya watu wamekuwa na vichwa vigumu kuachana na vitendo hivyo na badala yake kila kukicha wamekuwa wakiendesha vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wananchi wenzao, wasiostahili adhabu hiyo.

Mara kwa mara vitendo vya ukatili wa kijinsia vimekuwa vikisikika kutokea kwa wanawake, pamoja na watoto. Lakini pia kwa siku za hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu tunaambiwa baadhi ya wanawake nao wameonekana kuwa wanyama kwa kufanyia ukatili wa kijinsia waume zao.

Baadhi ya wanaume wamekuwa wakiwafanyia ukatili wa kijinsia wake zao, kwa sababu ya mfumo dume, kwa kuwapa kipigo kikali, ukatili wa kingono na ukatili wa kila aina kwa kutumia mfumo huo dume.

Aidha, watoto nao wamekuwa wakifanyiwa vitendo hivyo vya ukatili, vikiwemo vya kupigwa pindi wanapopatikana na makosa ambayo hata adhabu yake ilitakiwa kuonywa tu, kwa mfano mtoto anapokomba mboga chunguni ama kwa kusikia njaa ama vinginevyo, ama anapopoteza fedha alizopewa kwa ajili ya kununua kitu furani dukani, utakuta mzazi au mlezi anampatia adhabu kali ambayo haiendani kabisa na umri wake.

Wazazi au walezi wengine wamekuwa wakiwapatia adhabu ya kuwafunga na kamba mikono watoto wao na kisha kuwachoma na kuwasababishia majeraha mwilini.

Hali hiyo ya ukatili ndiyo inayoweza kumshinda mtoto husika na kuamua kukimbilia mitaani, na kuzalisha mtoto wa mitaani ambaye kwa namna nyingine maisha yanavyozidi kuwa magumu kwake hataimaye uamua kujiingiza kwenye makundi ya kiuharifu na kasha kuiishia jela au kuuawa na wananchi wanaojichukulia sheria mikononi pindi wanapomtuhumu kutenda kosa lolote la kiuharifu.

Lakini pia wazazi ama walezi wengine wamekuwa wakifanya ukatili kwa watoto, ambao ni wakuwanyima haki yao ya msingi ya kuwapatia elimu, ambayo ingemsaidia katika maisha yake ya baadaye.

Ama wazazi na walezi wengine wamekuwa wakiwatumikisha watoto wao ambao umri wao hasa unafaa kuwa shule kwa kazi ambazo haziendani na umri wao, kwani baadhi yao uwatumikisha katika kazi za mashambani, uwatumikisha katika kazi za uvuvi, uchungaji wa mifugo, kazi za migodini na kazi nyingine hatarishi kwa maisha yao.

Kwa mfano mimi hainiingii akilini kumtumikisha mtoto mwenye umri wa miaka saba katika kazi ya uvuvi, kwani ajali ya kuzama mtumbwi ikitokea, kamwe mtoto huyo hawezi kujiokoa kwa sababu hajui hata kuogelea kulingana na umri wake kuwa mdogo. Kwa jinsi hiyo hicho ni kitendo cha kumtoa kama sadaka mtoto mwenye umri huo.

Pia baadhi ya wanaume wanawafanyia vitendo vya ukatili wa kijinsia wake zao, kwani utakuta mwanaume kazi yake ni kukaa vijiweni tu muda wote akipiga soga, kuanzia asubuhi hadi jioni. Na kazi ya shambani au ya uzalishaji mali anamwachia mwanamke na watoto wake pekee.

Baadhi ya wanaume hao wamekuwa  ama wakikalia kulewa pombe tu na muda wa chakula unapowadia urejea nyumbani na kudai chakula tena kwa sauti kubwa, ilihali hajui chakula hicho kimedhalishwa kutoka wapi na hata hiyo mboga anayoitumia kulia hajui imenunuliwa na nani? Lakini bila soni mwaume mtu mzima ujikalisha kwenye meza na kuanza kubugia chakula hicho kana kwamba kakizalisha yeye.

Na kibaya zaidi anapokuta mwanamke hajaandaa chakula, ugeuka kuwa mbogo na kuanza kumtolea matusi na kejeri na hata kumshushia kipigo kikali kama kwamba ni mbwa mwizi.

Wakizungumza kwa nyakati na maeneo tofauti na mwandishi wa makala hii, baadhi ya wanawake wilayani Bunda, Mara, walisikika wakisema kuwa hata wakati wa mavuno, licha ya waume zao kutoshiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo hicho, waume zao wamekuwa wakinyang’anywa fedha zote walizouza mazao yao na kupewa kamgao kidogo tu, nyingi zikichukuliwa na waume zao na kwenda kufanyia mambo ya starehe ukiwemo unywaji wa pombe na vimwana vingine vya pembeni maarufu nyumba ndogo.

Mashirika pamoja na asasi mbalimbali za hapa nchini na hata nje ya nchi zimekuwa zikijitahidi  sana kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa ndani ya jamii yetu, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaoendesha vitendo hivyo.

Nao baadhi ya kina mama wamekuwa wakiwafanyia unyama usiovumiliwa watoto wao, tena wengine wakisikika wakisema si ni mwanganu hata kama ni kimuua. Labda hapa niwakumbushe akinamama wa aina hiyo kwamba mtoto ukisha mzaa ni wa serikali, iwapo ukimfanyia ukatili wa aina yoyote sheria itachukuliwa dhidi yako bila kujali kwamba wewe ndiye uliyemzaa.

Kutokana na elimu inayotolewa na mashirika, pamoja na asasi hizo, hivi karibuni serikali wilayani Bunda mkoani Mara, ililipongeza shirika lisilokuwa la kiserikali la Zinduka lililoko wilayani humo, linalofadhiliwa na shirika la The Foundation For Civil Society, kwa kuwapatia wananchi elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ili vitendo hivyo viweze kukomeshwa ndani ya jamii.

Pongezi hizo zilitolewa na mkuu wa wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili, aliyewakilishwa na katibu tarafa cha Nansimo, Jonas Nyaoja, kwenye mafunzo ya kupinga vitendo hivyo.

Mafunzo hayo ambayo yalikuwa ni mwendelezo wa mafunzo mengine ambayo yamekwishafanyika, yalifanyika katika ukumbi wa kituo cha walimu katika mji mdogo wa Kibara, uliko katika makao makuu ya jimbo la Mwiabara.

Mkuu huyo wa wilaya ya Bunda alisema kuwa serikali wilayani hapa inatambua mchango mkubwa wa shirika hilo katika kutoa elimu juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, ili jamii iweze kupata uelewa na kuachana na vitendo hivyo.

 “Serikali wilayani Bunda inatambua mchango mkubwa unaaotolewa na shirika hili la Zinduka katika kutoa elimu kwa jamii juu ya ukiukwaji haki na unyanyasaji wa kijinsia. Sasa elimu hii wananchi wetu wakiipata itawasaidia kubadilika na kuacha vitendo hivyo” alisema Nyaoja kwa niaba ya DC Bupilipili.

Aidha, baadhi ya wadau mbalimbali wanaopinga vitendo hivyo wilayani hapa, pia wamelishukuru shirika hilo kwa kuwapatia mafunzo hayo kwa sababu vitendo vya ukatili wa kijinsi vimekithiri sana ndani ya jamii yetu, ukiwemo ukatili wa kiuchumi pamoja na ule wa tendo la ndoa.

Wadau hao ambao ni pamoja na wazee wa mila, wazee maarufu, viongozi wa madhehebu ya dini, vyama vya siasa, watendaji wa vijiji na kata, pamoja na wenyeviti wa vijiji, walisema kuwa Shirika la Zinduka limejikita sanan katika kutoa elimu hiyo kwa jamii.

Waliyaomba mashairika mengine kuiga mfano huo, kwani wananchi wengi wamekuwa wakiendesha vitendo hivyo kwa sababu ya kukosa uelewa na kwamba ni shirika la kwanza kufika mkatika maeneo yao na kuwapatia elimu hiyo.

Walisema kuwa ukatili mwingine ni ubakaji wa wanawake, utumikishaji wa watoto wadogo kwenye shughuli hatarishi ambazo haziendani na umri wao, ukatili wa kutokupeleka watoto shule hususani wa kike, pamoja na unyanyasaji wanawake na wanaume ndani na hata nje ya ndoa.

Waliongeza kuwa ukatili mwingine ufanywa na wanaume kuachia shughuli za kilimo na uzalishaji mali wanawake tu, huku wanaume wengi wakikalia ulevi na uzululaji, ambapo nyakati za chakula ufika majumbani mwao na kudai chakula tena kwa kuamrisha, ambapo wanawake wanaposema hakuna chakula uambulia kichapo au matusi ya uzalilishaji.

Walisema kuwa wamridhika na mafunzo hayo ambayo yamewapatia mwanga, ambapo wataisambaza elimu hiyo katika maeneo yao ili jamii iweze kubadilika.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika la Zinduka, mhasibu wa shirika hilo, Godfrey Anatory, alisema kuwa wanatoa mafunzo hayo kwa makundi mbalimbali ya kijamii katika kata tisa za jimbo la Mwibara na kwamba katika awamu ya kwanza walitoa mafunzo hayo katika kata 13 za majimbo ya Bunda na Bunda mjini.

“Mafunzo haya tunayaendesha kwa kata tisa za jimbo la Mwibara, lakini pia mafunzo kama haya tulikwishayaendesha katika kata 13 za majimbo ya Bunda na Bunda mjini. Na baadaye tuendesha mafunzo haya kwa viongozi mbalimbali wakiwemo maasikari polisi, mahakimu na wanasheria, ili jamii iweze kujua athari za ukatili wa kijinsia na adhabu yake” alisema.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dk. Stanely Maendeka, alisema kuwa malengo ya mafunzo hayo ni kupata uelewa sahihi wa dhana za kijinsia na dhana ya ukatili wa kijinsia, na kupata uelewa na uwezo wa kutetea na kukomesha ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.

Dk. Mahendeka aliyataja maelengo mengine kuwa ni pamoja kurekebisha mapendekezo ya awali ya mradi, ili ibebe shughuli zinazogusa kukomesha ukatili wa kijinsia, kurekebisha bajeti iweze kuingiza au kuchukuwa shughuli zilizopendekezwa, kukomesha ukatili wa kijinsia na kuweza kutekeleza mradi vizuri zaidi na kupata matokeo yaliyotarajiwa.

Mkurugenzi wa shirika la Zinduka Maximillian Madoro, aliwaambia waandishi wa habari kuwa wamekuwa wakitoa mafunzo na elimu mara kwa mara kwa jamii, ili kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsi katika wilaya ya Bunda, mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla vitokomezwa.

Madoro amesema kuwa kupitia elimu hiyo kwa kiasi furani jamii imekwisha badilika na kuachana na vitendo hivyo ingawa bado kuna changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika baadhi ya wanajamii na kwamba pamoja na changamoto hizo wanaendelea kutoa elimu hiyo ili kufikia malengo yao ambayo kikubwa ni kutokomeza vitendo hivyo.

Kwa kumalizia makala yangu napenda kuwakumbusha wananchi wote kwamba tushirikiane na serikali pamoja na mashirika kama haya ya Zinduka, kupinga vitendo hivi vya ukatili wa kijinsia, kwani pia vinavunja haki za msingi za binadamu.

Wote kwa pamoja tukipiga kelele  na kukemea vitendo hivi, ikiwa ni pamoja na kuwafichua ama kuwataja bayana wale wote wanaoendesha vitendo hivi, vikiwemo na vile vya kukata watu wenye ualbino viungo vyao na kukata mapanga na kuwaua wazee wenye macho mekundu eti kwa imani ya ushirikina, hakika vita hii tutaishinda. Na kuwa na jamii iliyostarabika.

Pia tutowe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama, pindi tunaposhuhudia matukio kama hayo ndani ya jamii yetu, basi tuwe mstari wa mbele kutoa ushahidi mahakamani ili mhusika au wahusika waweze kuchukuliwa hatua na kuhukumiwa adhabu anayostahili kulingana kosa lake alilotenda kwa mjibu wa sheria za nchi yetu.


COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Makala ya Elimu
Makala ya Elimu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgI29IwtPF-zK9p6MQTEyuRz9cZv_fBKLmvtVeWnBuAorXLD8S8kQw0qhOB8h-IHH7WVt5uqb4NEbS425xRZKvfpOTpaCRB95tpwv1qM8-gYIwvyexa3iVRETb5YsutjgPTE-KNzCqRo9E/s640/Makala+2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgI29IwtPF-zK9p6MQTEyuRz9cZv_fBKLmvtVeWnBuAorXLD8S8kQw0qhOB8h-IHH7WVt5uqb4NEbS425xRZKvfpOTpaCRB95tpwv1qM8-gYIwvyexa3iVRETb5YsutjgPTE-KNzCqRo9E/s72-c/Makala+2.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/kutokana-na-vitendo-vya-unyanyasaji.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/kutokana-na-vitendo-vya-unyanyasaji.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content