Habari Mpya

Friday, 4 August 2017

WAKUU wa mbalimbali wa kapuni za utengenejaji magari nchini Ujerumani wamekubaliana mapema wiki iliyopita katika mkutano wa kilele uliowakutanisha na viongozi wa kisiasa kutumia kiasi cha Euro Milioni 500, sawa na Dola Milioni 592 katika kuboresha programu za kompyuta katika magari milioni 5.3 yanayotumia nishati ya dizeli.


Mkutano huo ni sehemu ya juhudi za kurejesha imani kwenye sekta hiyo ilikuwa imechafuliwa.Huku kampuni za kutengeneza magari yalionekana kujiweka kando juu ya shinikizo la kisiasa lililotaka mabadiliko ya gharama kubwa zaidi za vifaa

Watengenezaji hao wa magari waliokutana mjini Berlin, Volkswagen, pamoja na chapa zake za kifahari Audi na Porsche, BMW, Daimer, Ford ya Ujerumani na chapa inayomilikiwa na kampuni ya Ufaransa, Opel, walikubalina kuboresha programu hizo kama sehemu ya hatua za mfululizo za kushughulikia mzozo unaovikabili viwanda vinavyotengeneza magari yanayotumia dizeli.

Barbara Hendricks ambaye ni Waziri wa Mazingira alisisitiza uboreshaji wa programu yalikuwa ni hatua ya awali kuelekea kuboresha viwango vya uchafuzi wa hali ya hewa hewa. Na kukiri mbele ya waandishi wa habari baada ya mkutano huo kwamba maazimio yaliyoazimiwa katika mkutano huo hayatajitosheleza.

Waziri Mkuu wa Jimbo la Kati la Lower Saxony, ambako ndiko makao ya kampuni ya magari ya Volkswagen, Stephan Weil yaliko alisema msukumo wa kuboreshwa kwa programu hizo utaendelea.
mwezi Septemba 2015, Sekta ya magari iliyumba wakati Volkswagen ilipokiri kufunga vifaa kwenye magari yake ambavyo vinatoa taarifa za uongo za vipimo vya nishati ya dizeli katika uchafuzi wa mazingira kwa zaidi ya magari milioni 11 duniani kote.
Mzozo huo uliongezeka baada ya vyombo vya habari kuripoti kuhusu makampuni matano ya magari, Volkswagen, Audi, Porsche, BMW na Daimler, yalikuwa yameunda genge la siri la wafanyabiashara ambao miongoni mwa mambo mengine hujadiliana kuhusu viwango na namna ya kudhibiti utoaji wa gesi chafu tangu miaka ya 1990.
Utafiti wa maoni uliotolewa na taasisi ya YouGov siku za hivi karibuni ulionyesha kuwa ni asilimia 41 tu ya Wajerumani wenye imani ya sekta ya magari, ambayo inaajiri watu 828,000, inayowakilisha asilimia 14 ya nguvu kazi kwenye sekta ya uzalishaji nchini Ujerumani.

Mkutano huo pia uliunda sehemu ya maandalizi ya uchaguzi wa shirikisho la Ujerumani utakaofanyika Septemba 24, huku chama cha Kansela Angela Merkel cha CDU kikikosolewa kwa kuendeleza uhusiano uliopitiliza na watengenezaji wa magari na namna kilivyoshughulikia mzozo wa uchafuzi wa hali ya hewa.

Mkutano huo ambao ulihudhuriwa na mawaziri wakuu wa majimbo matano ya Ujerumani ambako ndiko yaliko makao makuu ya kampuni ya magari hayo pia uliadimia kutoa kiasi cha Euro Milioni 500 kushughulikia matatizo ya uchafuzi wa mazingira ya mijini, na  kuanzisha mfuko wa ruzuku unayolenga kuboresha na kuendeleza mifumo ya usafi kwenye sekta ya usafiri.



Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -