Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Ufuta Na Mihogo kuinufaisha Lindi

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi ameiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kukopesha wakulima wa mazao ya ufuta na mihogo i...

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi ameiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kukopesha wakulima wa mazao ya ufuta na mihogo ili waweze kulima kilimo cha kisasa na cha kibiashara hasa kwa wakulima wadogo wadogo wa mkoani humo.
Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi

Zambi alitoa wito huo wakati wa mkutano wa Wadau wa Korosho na Ufuta Mkoa wa Lindi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Zambi alisema kuwa mkoa wa Lindi ni mkoa uliojaaliwa katika kuzalisha mazao ya ufuta na mihogo lakini changamoto kubwa ni mtaji wa kulima kibiashara ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

“Wakulima wa mkoa wa Lindi wapo tayari kushiriki katika kuleta mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara lakini kwa sasa suala la mtaji wa kilimo cha kibiashara ni changamoto kubwa,” alisema Zambi.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Lindi alisema kuwa ili kuwezesha wakulima hao kulima kibiashara Benki ya Kilimo ina wajibu wa kutoa mikopo yenye riba nafuu ili kuhamasisha wakulima hao wa mkoa wa Lindi waweze kuongeza uzalishaji wenye tija katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini mkoani humo.

Aliongeza kuwa kama TADB itaboresha upatikanaji wa mikopo na huduma za kifedha kwenye miradi ya maendeleo ya Kilimo kwa riba nafuu zilizo chini ya viwango vya kibiashara kwenye soko kutawezesha wakulima wa Tanzania kufikia uchumi wa kati kama ilivyolengwa na Serikali ifikapo mwaka 2015.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Francis Assenga alisema kuwa Benki ya kilimo ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima wadogo wadogo waliokuwa kwenye vikundi ili waweze kukopeshwa.

Assenga aliongeza kuwa Benki ya Kilimo pia ipo tayari kuwekeza kwenye miradi ya maendeleo ya Kilimo kwa kuipatia mikopo yenye riba nafuu zilizo chini ya viwango vya kibiashara kwenye soko.

“Kwa kutambua umuhimu wa wakulima wadogo wadogo nchini TADB imedhamiria na kujizatiti kuhakikisha inachangia kwa kiasi kikubwa katika  kuleta Mapinduzi yenye tija katika Sekta ya Kilimo nchini kwa kusaidia upatikanaji na utoaji wa fedha ikiwa ni pamoja sera nzuri zitakazosaidia maendeleo ya kilimo nchini,” alisema.

Kaimu Mkurugenzi huyo alisema kuwa Benki yake inaandaa mfumo mahususi wa uratibu kwa kushirikiana na halmashauri za mikoa ili kuhakikisha kuna upatikanaji wa fedha kwa ajili ya minyororo ya ongezeko la thamani kwa mazao ya Kilimo nchini.

“Tupo tayari kusaidia uzalishaji kwenye hatua mbali mbali za uongezaji wa thamani, hadi masoko ya bidhaa za mwisho  hadi kumfikia mlaji na kusaidia kuwaunganisha wakulima na masoko kupitia halmashauri zao,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Augustino Chacha alisema kuwa TADB inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma zisizo za kifedha kwa wakulima kama vile kujengewa uwezo juu ya uandaaji wa andiko la miradi ya Kilimo, pamoja na upatikanaji wa taarifa za masoko, usimamizi wa biashara, mafunzo juu ya miradi ya Kilimo na mbinu za majadiliano ya mikataba.

 “Tupo tayari kutoa mikopo kwa ajili ya kuwanyanyua wakulima kama ilivyolengwa na Serikali kupitia mikopo ya pembejeo kuongeza tija kwenye uzalishaji, miundo mbinu ya umwagiliaji na ununuzi wa zana za kilimo,” alisema.

Chacha aliongeza kuwa kwa upande wa mikoa ya kusini Benki ya Kilimo imejipanga kueendeleza miundombinu ya umwagiliaji na maghala pamoja na uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya korosho na mihogo na kuimarisha viwanda vya kubangua mazao ya korosho, na kusindika ufuta, mihogo.
Chacha aliongeza kuwa Benki imejipanga kuwezesha uanzishaji wa mashamba mapya na ya kisasa ya mihogo, korosho na ufuta mkoani Lindi.


COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Ufuta Na Mihogo kuinufaisha Lindi
Ufuta Na Mihogo kuinufaisha Lindi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEio0JQ4hts6m0IX4czM9KBYtPbUJ7MUanBskj3cpQNs8xabutB0Wd4oDNtmKhBmZhGF-24xXTSPgnTpRG3D6lE7pJp_aTf1asy_LBFUeqazh0_cgGd_0qTltGuqs-5XSjY5_Jg0kgS0eOg/s640/Zambi+mkuu+wa+mkoa+Lindi.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEio0JQ4hts6m0IX4czM9KBYtPbUJ7MUanBskj3cpQNs8xabutB0Wd4oDNtmKhBmZhGF-24xXTSPgnTpRG3D6lE7pJp_aTf1asy_LBFUeqazh0_cgGd_0qTltGuqs-5XSjY5_Jg0kgS0eOg/s72-c/Zambi+mkuu+wa+mkoa+Lindi.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/ufuta-na-mihogo-kuinufaisha-lindi.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/ufuta-na-mihogo-kuinufaisha-lindi.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content