Habari Mpya

Habari Zote

Archive for May 2026

Bei ya mafuta ghafi duniani imeendelea 22.7 ikilinganishwa na dola 112.9 zilizorekodiwa Aprili 7, 2026, mabadiliko makubwa katika soko la nishati duniani.


Hata hivyo, kushuka huku bado hakujafikia WaTanzania. Wataalamu wanasema bei za rejareja za petrol na diseli nchini zinaweza kuanza kushuka taratibu wiki zijazo kutokana na mzunguko wa gharama za usafirishaji, bima na tozo za serikali kabla ya kufikia mlaji wa mwisho.


EWURA hufanya marekebisho ya bei kila mwezi tarehe 1. Serikali kupitia Wizara ya Nishati imesema iwapo mwenendo huu utaendelea, basi kuna uwezekano wa kupungua kwa shinikizo la gharama za nishati nchini katika wiki na miezi ijayo.

Mazungumzo na Himid Mao Yaanza, Yataka Pesa Ndefu"

Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania, Azam FC wameanza rasmi mazungumzo na kiungo wao mkabaji Himid Mao kwa lengo la kumpa mkataba mpya kabla ya msimu wa 2026/2027. Hatua hiyo inakuja huku tetesi zikidai kuwa wapinzani wao Simba SC wanyatia huduma ya nyota huyo aliyerejea klabuni hapo msimu uliopita.

Chanzo cha ndani klabuni hapo kimeiambia Lenzi Media kuwa ingawa Azam wapo mbele ya Simba katika kumsajili Mao, kiungo huyo anataka ongezeko kubwa la mshahara ikilinganishwa na mkataba wa mwaka 1 aliosaini aliporejea. “Tayari mazungumzo mapya yameanza, lakini si rahisi kwani anahitaji pesa ndefu. Viongozi wanaendelea kuzungumza naye,” kilisema chanzo hicho.

Mao alicheza Azam FC kuanzia 2008 hadi 2018 kabla ya kuelekea Misri kuichezea Petrojet, ENPPI, Ghazl El Mahalla na Tala’ea El-Gaish SC hadi 2025.

 Akizungumzia usajili huo, staa wa zamani wa Azam Erasto Nyoni anayeichezea Kagera Sugar amesema: “Kiwango cha mchezaji ndiyo thamani ya pesa yake. Mao amewaonyesha Azam kwa vitendo kuwa bado ana kiwango cha juu.”

Chanzo: Azam FC  
NA: PETER MWAMKMBA

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -