Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

MOBILE COURT YAANZA KUWASAKA WACHAFUZI WA PAMBA.

Bodi ya Pamba Tanzania wilayani Maswa mkoani Simiyu imefanya operesheni maalumu ya kuwakagua wanunuzi na wauzaji wa Pamba ambao wamekuwa wa...

Bodi ya Pamba Tanzania wilayani Maswa mkoani Simiyu imefanya operesheni maalumu ya kuwakagua wanunuzi na wauzaji wa Pamba ambao wamekuwa wakichafua  zao hilo kwa  kuichanganya mchanga, maji na udongo ili kuongeza uzito na kupata faida mara mbili ambapo katika huku oporesheni wakulima na wanunuzi wamepongeza zoezi hilo linaloondoa udanganyifu katika zao hilo.

Wakiongea katika ukaguzi huo baadhi ya wanunuzi na wakulima katika vijiji vya Mwabayanda na Nguliguli walisema kuwa zoezi hilo ni zuri kwa sababu linawafanya wajitathini na kufahamu ubora wa pamba wanayoinunua pia kuwakumbusha wakulima kutoharibu pamba yao.
Kampuni ya Kahama Cotton Co Ltd ya mjini Kahama mkoani Shinyanga

‘’zoezi hili tunaomba liwe endelevu kwa sababu linagusa wakulima na wanunuzi kuwa yoyote atakayekutwa na kosa anahukumiwa hapohapo, litaondoa uchafuzi wa pamba na kuongeza ubora wake hivyo litakuza soko la pamba kimataifa ambayo awali ilikuwa imeshuka kutokana na pamba yetu kuwa chafu’’ alisema Nkuba Minoja.

John Ng’hona alisema kuwa pamoja na ukaguzi huo, katika msimu ujao watuletee  mbegu ya pamba na pembejeo kwa wakati ili tuweze kulima kwa uhakika na kuongeza uzalishaji.

‘’tulikuwa tukiletewa mbegu zisizoota hapo awali, dawa isiyouwa wadudu…hivyo tunaomba wazingatie haya ili wakulima waweze kuona thamani ya zao hili pia tuongezewe maafisa ugani ili waweze kuwafikia wakulima kuwashauri kulima kitaalamu’’ alisema Mtemi Ndahya.

Naye Mkaguzi wa Bodi ya Pamba wilayani humo Ally Maborouk alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu na wanunuzi wanaoharibu pamba ni bora watafute biashara nyingine kwa kuwa bodi hiyo inasimamia wauazaji na wanunuzi na kuhakikisha pamba inayozalishwa na kuuzwa ni safi.

‘’wanunuzi wanaoharibu pamba ni bora watafute biashara nyingine, tutahakikisha pamba yote inayozalishwa na kuuzwa ni safi ili isiharibu soko la zao hilo kimataifa, tuko imara tutahakikisha tunawashughilikia ipasavyo’’ alisema Maborouk.

Aidha katika zoezi hilo lilioambata na mahakama  inayotembea (mobile court) imekagua vituo vya pamba katika vijiji vya Nguliguli, Mwabayanda, Ilimbambasa, Senani, Zebeya na Mwabadimi na kuibua hoja baada ya mnunuzi mmoja wa pamba kampuni ya Gaki kijiji cha Igumangobo kufunga kituo na kuwakimbia wakaguzi hao.

Baada ya kuona hali hiyo Mkaguzi wa Pamba aikifunga kituo hicho na kumwagiza mtendaji wa kijiji kumkamata mnunuzi huyo ili aweze kueleza sababa zilizomfanya akikimbie kituo chake.

Katika kijiji hichohicho cha Igumangobo wanunuzi wawili Malugu Sungwandeba na George Salum wanunuizi wa pamba Kampuni ya Kahama Cotton Co Ltd ya mjini Kahama mkoani Shinyanga walipatikana  na hatia baada ya kukiri kukutwa wamenunua pamba chafu katika ghala lao


Katika mahakama hiyo inayotembea Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Nyalikungu,Lilian Kinyemi aliwahukumu washitakiwa hao adhabu ya kifungo cha miezi mitatu jela kila mmoja au kulipa faini ya Sh 50,000 na Kampuni hiyo kuilipa bodi ya Pamba Sh 500,000 na washitakiwa walilipa faini zote na kuachiwa huru.

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: MOBILE COURT YAANZA KUWASAKA WACHAFUZI WA PAMBA.
MOBILE COURT YAANZA KUWASAKA WACHAFUZI WA PAMBA.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXTw82Xu34vF5wYrU4yRkSBxJ478XEpPvY14336CRVvQDvVQbQdRdj0iqM5WxG_pUcmPZPgiuhzwebz1Dd5v9y8mBym_ys1Y5kzG0aifZsF6gXqtfpOuU52IUyDChc4yVQ2NBy-BLuvLo/s640/Snapshot.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXTw82Xu34vF5wYrU4yRkSBxJ478XEpPvY14336CRVvQDvVQbQdRdj0iqM5WxG_pUcmPZPgiuhzwebz1Dd5v9y8mBym_ys1Y5kzG0aifZsF6gXqtfpOuU52IUyDChc4yVQ2NBy-BLuvLo/s72-c/Snapshot.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mobile-court-yaanza-kuwasaka-wachafuzi.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mobile-court-yaanza-kuwasaka-wachafuzi.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content