Habari Mpya

Friday, 4 August 2017

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu nchini (LHRC) kimesema kuwa mkoa minne ndani chini inaongoza kwa ukiukwaji wa ukiukwaji wa haki za wanawake na watoto unaofanyika kupitia ukatili wa kijinsia, kingono, ulawiti, unajisi, ukeketaji na unyanyapaa.

 Mkurugenzi  Mtendaji wa LHRC, Hellen Kijo-Bisimba alisema matukio hayo yameshamiri katika mikoa ya Tabora, Dar es Salaam, Mbeya na Iringa bado yameonekana  kuendelea kuwa tishio kwa ustawi wa jamii.
Mkurugenzi  Mtendaji wa LHRC, Hellen Kijo-Bisimba akiongea na wandishi wa habari

“Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa tumegundua kwamba mikoa hiyo bado inaongoza kwa ukiukwaji wa haki za wanawake na watoto”

Bisimba alisema jeshi la polisi linapaswa kukomesha vitendo hivyo kubadilisha mbinu za kiutafiti na upelelezi wa kesi mbalimbali ili kuhakikisha watuhumiwa wanaopatikana wanachukuliwa sheria kali.

 Ameongeza kwamba kipindi cha nusu mwaka  hali ya haki za binadamu nchini bado ni mbaya ikilinganishwa na miaka iliyopita.

Haliyo imesababishwa na ukiukwaji wa haki za kiraia, kisiasa, haki ya kuishi, kuminywa kwa haki na uhuru wa kujieleza pamoja na kuzuiwa kwa haki ya kukusanyika.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -