Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

WAZIRI MKUU ASEMA ATAFWATILIA KWA KINA UJENZI WA MIRADI YA MAJI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atahakikisha anafuatilia kwa kina ujenzi wa miradi mbalimbali nchini ikiwemo ya maji ili kuhakikisha ka...

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atahakikisha anafuatilia kwa kina ujenzi wa miradi mbalimbali nchini ikiwemo ya maji ili kuhakikisha kama inalingana na thamani halisi ya fedha zinazotolewa katika kugharamia miradi hiyo.

 Alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Julai 31, 2017) alipozungumza na wananchi wa Jiji la Mbeya katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Ruanda Nzovwe jijini Mbeya akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mbeya.
Waziri Mkuu alisema Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, inayolenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 imetenga sh. bilioni 237.8 kugharamia miradi ya maji nchini.
Alisema atafuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa ujenzi wa miradi yote ya maji nchini ili kuhakikisha malengo ya kampeni hiyo ya kuwafikishia wananchi huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao yanatimia.

“Nitafuatilia katika maeneo yote nchini ili kujua kama kiasi cha fedha kilichotolewa kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maji iwapo kinalingana na thamani halisi ya miradi husika. Lengo ni kuhakikisha kwamba thamani ya miradi yote inalingana na kiasi cha fedha kilichotolewa.”
Alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 mkoa wa Mbeya umetengewa sh. bilioni 10.383  kwa ajili ya utekelezaji miradi ya maji, ambapo kati yake sh. bilioni 1.693 zinatarajiwa kutumika kwenye Halmashauri ya Jiji la Mbeya huku sh. milioni 622.049 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maji ya Halmashauri ya wilaya ya Mbeya.

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi umuhimu wa kuzingatia sheria ya Mazingira inayozuia kufanya shughuli za kibinadamu pamoja na kujenga kwenye maeneo yote ya vyanzo vya maji ndani ya mita 60 ili kuliepusha Taifa kugeuka jangwa.

 Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwataka wananchi kuendelea kutekeleza kwa vitendo kauli ya Rais Dkt. Magufuli ya Hapa Kazi Tu kwa kufanya kazi kwa bidi ili kuweza kujiletea maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.


Majaliwa alitoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Mheshimiwa Joseph Mbilinyi kumuomba Serikali iruhusu mikutano ya hadhara kwa ajili ya viongozi wa vyama vya siasa, ambapo alimweleza kwamba hakuna kiongozi aliyezuiwa kufanya mikutano katika eneo lake la kiutawala.

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: WAZIRI MKUU ASEMA ATAFWATILIA KWA KINA UJENZI WA MIRADI YA MAJI
WAZIRI MKUU ASEMA ATAFWATILIA KWA KINA UJENZI WA MIRADI YA MAJI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgf5NdXa4qf1650uAjmNCj5H4r536uJ2wS6yzE1woTdwA_L51wQNBWvdbDI7g6cmBLzffKbRDceTiGdszDuwaLBAzDOU-TG3zTM-e3_MXZmdLMLcsLVaGW8rtIQfcJrgggR1BaSHkd2sSs/s320/PMO_6673.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgf5NdXa4qf1650uAjmNCj5H4r536uJ2wS6yzE1woTdwA_L51wQNBWvdbDI7g6cmBLzffKbRDceTiGdszDuwaLBAzDOU-TG3zTM-e3_MXZmdLMLcsLVaGW8rtIQfcJrgggR1BaSHkd2sSs/s72-c/PMO_6673.JPG
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/waziri-mkuu-asema-atafwatilia-kwa-kina.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/waziri-mkuu-asema-atafwatilia-kwa-kina.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content