Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Mpango wa Equip wainua kiwango cha elimu

https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mpango-wa-equip-wainua-kiwango-cha-elimu.html KATIKA kuinua kiwango cha elimu kwa shule za msingi a...

https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mpango-wa-equip-wainua-kiwango-cha-elimu.htmlKATIKA kuinua kiwango cha elimu kwa shule za msingi ambazo zilikuwa hazifanyi vizuri kitaaluma, serika liiliamua kuanzisha mpango wa kuinua ubora wa elimu Tanzania (Equip) katika shule hizo ambapo halmashauri ya mji wa Bunda iliyoko katika mkoa wa Mara, ni kati ya halmashauri ambazo zinatekeleza mpango huu.

Halmashauri hiyo yenye shule za msingi za serikali ziapatazo  61 na shule binafsi zipatazo tano, zinatekeleza mpango huo lengo likiwa ni kuhakikisha kiwango cha elimu katika shule hizo kinaboreka.

 Mpango huu wa kuinua ubara wa elimu Tanzania una malengo mengi yakiwemo ya kuinua ubora wa elimu na taaluma kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na kuleta maendeleo katika sekta ya elimu.

 Katika shule za halmashauri ya mji wa Bunda, tangu mpango huo ulivyoanza kutolewa mwaka 2015 tayari mafanikio mengi yamekwishaanza kupatikana na kuleta matokeo chanya ya kielimu, hali ambayo imeleta faraja kubwa kwa wazazi, walezi, wanafunzi, walimu, pamoja na wadau mbalimbali wa elimu katika halmashauri hiyo.

Mpango huu mbali na kuinua kiwango cha taaluma katika shule hizo, pia umewezesha wanafunzi kufanya kazi za kujitegemea pindi wawapo shuleni na hata majumbani mwao, kwa kulima kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula, pamoja na bustani za mboga na matunda.

Chakula wanachozalisha wanafunzi hao kwa kutumia nguvu zao wenyewe pamoja na mboga na matunda hayo wamekuwa wakiyatumia wakati wakiwa shuleni, pamoja na nyumbani kwao kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha afya zao.

Shule tatu za halmashauri ya mji wa Bunda, ambazo ni pamoja na shule ya msingi Mazoezi, iliyoko katika chuo cha ualimu Bunda, shule ya msingi Ushashi na shule ya msingi Mugaja, ambayo ni shule mama ya shule mpya ya Mbugani ni kati ya shule zilizoko katika mpango huo na tayari zimekwishayapata mafanikio makubwa, ya kuchumi, kiafya na kitaaluma.

Bonji Emmanuel Bugeni ni afisa maendeleo ya jamii katika halmashauri ya mji huo, anaelezea kuwau mpango huo, ambapo kikubwa ni kuinua kiwango cha elimu katika shule hizo pamoja na kuanzisha miradi ambayo itaziwezesha shule husika kutatua changamoto mbalimbali kupitia njia ya kujitegemea, ikiwa ni pamoja na kuwapatia chakula wanafunzi.

Anasema kuwa kupitia mpango huo shule ya msingi Ushashi kwa sasa wanao mradi wao wa kilimo cha mazao ya chakula, ambao umewasaidia watoto kupata chakula pindi wawapo shuleni hapo.

Aliongeza kuwa pia afya za watoto wanaosoma katika shule hizo kutokana na lishe bora wanayopata zimeboreka kwa kiasi kikubwa na kwamba pia hali ya utoro kwa wanafunzi umepungua sana na sasa watoto wanaipenda elimu.

Alibainisha kuwa hali ya ufundishaji kwa walimu pia imeboleka sana kwani walimu wamepata mori na hali na bidii katika kuwafundisha wanafunzi imeongezeka kwa kiwango kikubwa na walimu wanaonesha kuipenda kazi yao.

Aidha, anasema kuwa pia shule ya msingi Mazoezi nayo inao mradi wa kilimo cha Bustani ya mboga na matunda, mradi ambao pia umeshirikisha wazazi, walimu na wanafunzi, ambapo pia wanafunzi wamekuwa wakipatiwa mboga na kwenda nazo nyumbani kwao kwa ajili ya kuboresha afya zao na za wazazi wao pia.

“Wanafunzi pia wamekuwa wakipewa mboga kwa zamu zamu na kwenda nazo majumbani kwao, kwa ya kuzitumia pamoja na wazazi wao hapo nyumbani” alisema Bonji Emmanuel Bugeni afisa maendeleo ya jamii wa halmashauri ya Mji huo.

Anasema kuwa kuna shule mpya ya Mbugani ambayo ilianzishwa kwa malengo mahususi likiwemo la kuokoa maisha ya watoto waliokuwa wanatembea umbali mrefu na kuvuka barabara kuu ya Mwanza-Musoma ambapo baadhi yao walikuwa wakigongwa na vyombo vya moto pindi wanapovuka katika barabara hiyo ya lami.

Anasema kuwa mpango huo ndio uliosababishwa kuanzishwa kwa shule hiyo, ambapo wazazi, kamati ya shule, walimu na wananchi kwa ujumla waliweka mikakati kadhaa ya kujenga shule hiyo kwa kutumia nguvu zao.
“Huu mradi ni mkombozi katika suala zima la elimu na lishe kwa wanafunzi wetu, pamoja na maisha yao. Kulikuwa na changamoto nyingine ya wanafunzi kugongwa na vyombo vya moto wakati wakivuka barabara kuu ya Mwanza-Musoma wakati wa kwenda na kutoka shuleni.

“Hali hiyo iliwafanya wazazi, kamati ya shule pamoja na walimu kwa ujumla kukaa na kuanzisha wazo la kujenga shule nyingine ya Mbugani. Lakini pia hali hiyo iliasaidia kuondoa msongamano wa wanafunzi katika shule mama ya Mugaja” alisema Bonji Bugeni.

Halikadhalika afisa maendeleo huyo wa jamii alielezea changamoto zinazowakabili, ikiwemo ya kutokuwa na vyombo vya usafiri kutokana na halmashauri hiyo kuwa changa.

Lakini pia pamoja na maendeleo hayo aliwataka wazazi na walezi kuwa karibu zaidi na walimu kwani ni walezi wazuri wa watoto wao, kwa sababu muda mwingi wao ndio wanaokaa na watoto pindi wawapo shuleni kwao.

Alisema kuwa wazazi wanapokuwa karibu na walimu ikiwa ni pamoja na kufuatilia masomo ya watoto wao pamoja na mienendo yao, itawafanya walimu nao kuwa karibu na wazazi na wote kwa pamoja kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu na maarifa yanayotakiwa kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.

Naye afisa elimu vielelezo katika halmashauri ya mji huo Christina Lubaka, alisema kuwa mpango huo umeleta mafanikio makubwa katika shule hizo, ambapo anatoa mfano wa shule ya msingi Mazoezi ambayo imekuwa ikitekeleza miradi mingi ya kiuchumi.

“Kwa mfano wa shule moja tu ya Mazoezi ambayo iko kwenye chuo cha ualimu Bunda, imekuwa ikifanya vizuri katika miradi mbalimbali ya kuchumi, ambapo bidhaa wanazozalisha mashambani baadhi imekuwa ikiuzwa na kupata mahitaji mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kununua chaki” alisema Christina Lubaka afisa elimu vielelezo halmashauri ya mji wa Bunda.

Kaimu afisa elimu wa halmashauri ya mji wa Bunda, Undi Tanga, anathibitisha kuwepo kwa maendeleo makubwa ya kiucumi, kielimu na kitaaluma kwa ujumla katika shule hizo zote 66 za msingi katika halmashauri hiyo tangu mpango huo uanze kutekelezwa.
Tanga anasema kuwa kutokana na mpango huo ulioanzishwa mwaka 2015, kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu katika mikoa iliyofanya vibaya hapa Tanzania, ukiwemo na mkoa wa Mara, umesaidia kwa kiasi kikubwa kuinua taaluma katika shule hizo, ikiwa ni pamoja na kupunguza hali ya utoro kwa wanafunzi.

Alisema kuwa kwa jinsi hiyo utaona kwamba kuna mafanikio mengi sana yaliyotokana na mpango huu.

Alifafanua kuwa mpango huo wa kuinua ubora wa elimu Tanzania ulianzishwa na serikali katika mikoa ambayo ilionekana kufanya vibaya kielimu na kwamba halmashauri ya Mji huo nayo iliingizwa katika mpango huo ambao lengo lake kubwa ni kuhakikisha kiwango cha ubora wa elimu unakuwa juu.

Tanga alisema kuwa pamoja na kuboresha afya za wanafunzi kupitia miradi ya kilimo cha vyakula, matunda na mboga, lakioni pia kiwango cha taaluma kipanda kwa asilimia kubwa, sanjari na utoro kupungua, ambapo kabla ya mradi mahudhuri kwa wanafunzi katika shule hizo yalikuwa ni wastani wa asilimia 62 tu, lakini kwa sasa ni zaidi ya asilimia 90.

“Tangu mpango huu ulipoanza kutekelezwa katika shule za halmashauri yetu kwa ujumla tumekwishapata mafanikio mengi sana kwa ujumla.

Mafano utoro umepungua sana katika shule zetu, maana kabla ya mradi huu mahudhurio shuleni kwa wanafunzi yalikuwa ni wastani wa asilimia 62, lakini kwa sasa ni zaidi ya asilimia 90” alisema.

Anasema kuwa kabla ya kuanza kutekelezwa mpango huo katika shule zote kwanza ulianza uhamasishaji kwa wazazi, walimu, kamati za shule na wadau mbalimbali wa maendeleo, lengo likiwa nikutaka kufikia malengo yaliyotarajiwa.

Alisema kuwa pia walimu walipatiwa mafunzo ya masomo mbalimbali yakiwemo yale ya KKK yaani kujua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu, ambapo pia kamati za shule zilipatiwa mafunzo rasmi ili ziweze kupata uelewa kuboresha elimu katika shule zao.

Aliongeza pia katika kufikia malengo hayo vilabu mbalimbali vya wanafunzi, hususani vya kuhusu afya, elimu ya kutigemea na mambo kadha wa kadha vilianzishwa katika shule hizo, ambapo kupitia vilabu hivyo wanafunzi walifundishwa mambo mbalimbali ya kuwajengea uwezo wa kiakili na kimaarifa.

Kufuatia maendeleo hayo Tanga anatoa wito kwa wazazi, kamati za shule na walimu wote kwa pamoja kushirikiana ili kuinua kiwango cha elimu katika shule hizo, kwani elimu ndiyo ufunguo wa maisha.

Nao baadhi ya walimu wa shule za msingi katika halmashauri ya mji wa Bunda, walielezea furaha yao kuhusu mpango huo, pamoja na kuelezea mafanikio ambayo wamekwishayapata kwamba ni mengi sana, ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati kadhaa ambayo imewasaidia kuinua kiwango cha elimu katika shule zao.

Mwalimu Madaraka Rusarika ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ushashi, ambaye anabainisha wazi kwamba kwa ujumla mpango huo umewaletea maendeleo mengi sana katika shule yao, huku akiishukuru serikali kwa ubunifu huo. 

Lakini pamoja na mafanikio hayo mwalimu huyo anasema kuwa kuna changamoto kadhaa ambazo inabidi zifanyiwe kazi, ikiwemo ya baadhi ya wananchi kuingilia mipaka na shule na kuendesha shughuli za kibinadamu, ambapo anatoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kuingilia mipaka ya shule.

Nao baadhi ya wazazi wanaelezea mikakati waliyoifanya kwa ushirikiano wa  walimu kwa pamoja na kufikia mafanikio ambayo wanayo kwa sasa katika kuboresha elimu katika shule hizo.

Joseph Mtara ni mwenyekiti wa kamati ya shule Ushashi na Wasato Nyamsha ni mzazi na mjumbe wa kamati ya shule hiyo ambao wanasema kuwa umoja wao kati ya kamati ya shule, wazazi na walimu kwa ujumla ndicho chanzo cha mpango huo kufikia malengo yake ya kuinua ubora wa elimu katika shule hiyo ya Ushashi.

Katika shule ya msingi Mazoezi, ambayo pia ni kati ya shule zinazonufaika na mpango huo, mwalimu mkuu wa shule hiyo Vicent Ndunguru, anaelezea mradi wao wa bustani jinsi unavyowasaidia  katika shule hiyo, ambapo pia anatoa pongezi kwa serikali kwa kutoa elimu bure. 
Baadhi ya wazazi waliozungumza na mwandishi wa makala hii wanaendelea kuelezea kuhusu ushirikiano wao na walimu kupitia umoja wao wa unaojulikana kwa jina UWW, kwamba ndicho chanzo kikuu cha mafanikio na kwamba kupitia mpango huo majumbani mwao pia wana miradi hiyo ya kilimo cha mboga na matunda kwa ajili ya kuboresha afya zao.

“Kupitia mpango huu wa Equip hata sisi umetusaidia sana tukiwa kama wazazi, maana tumeanzisha bustani za mboga na matunda ambayo kwa sasa utusaidia kuboreesha afya zetu maana  tunapata lishe bora sisi na watoto wetu” alisema Lugembe Lugembe, ambaye ni mratibu wa ushirikiano (UWW) shule ya msingi Mazoezi.

Mwandishi wa makala hii alipata fursa ya kutembelea shule ya msingi Mugaja na kuzungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Mwaliki Biseko, ambaye anaelezea changamoto zilizokuwa zinawakabili kabla ya mpango huo kuanza kutekelezwa shuleni hapo, kwamba zilikuwa nyingi, ikiwa ni pamoja na utoro na matokeo kutokuwa ya kuridhisha, ambapo kwa sasa hali imebadilika kwa kiasi kikubwa kwani m afanikio ni mengi sana.

Naye Daudi Masalu ni mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Mugaja pamoja na baaadhi ya wazazi wengine wao pia wanaelezea mikakati hiyo ikiwemo ya kuanzisha shule nyingine mpya ili kukabiliana na changamoto mbalimbali, ikiwemo ya kujenga shule mpya ya Mbugani.

Katika hatua nyingine mtoto Nacy January, aliyepata ajali wakati akivuka barabara akiwa anakwenda shuleni, pamoja na mama yake mzazi Joyce Willison, walielezea changamoto iliyokuwepo kwam kutokuwa na shule katika eneo hilo, ambapo kwa sasa motto huyo anasoma katika hiyo shule mpya tena kwa ukaribu zaidi.

Hata hivyo mama yake anaiomba serikali kuendelea kuiboresha shule ya msingi mbugani, ili iweze kupata mahitaji yote kwa kuongeza vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na miundombinu nyingine mbalimbali.

“Nilipata ajali nikagongwa na bodaboda wakati nikivuka barabara ya lami kwenda shuleni lakini nilikaa nyumbani nikitibiwa lakini sasa nashukuru Mungu nilipona na sasa naendelea na masomo yangu katika hii shule.

Nashukuru sana serikali kuleta mpango huu ni mkombozi kwa sisi wanafunzi” alisema Nacy aliyegongwa na bodaboda akiwa darasa la pili mwaka 2013 ambapo hali hiyo ilisababisha baada ya kupona arudi nyuma darasa moja ambapo sasa katika shule hiyo mpya.

Kwa ujumla serikali imekuwa na mipango kadhaa ya kuhakikisha watoto wanapata elimu inayostahili ambayo itawasaidia katika masiaha yao ya baadaye, ukiwemo mpango huu wa Equip ambao lengo lake ni kuinua ubora wa elimu kwa shule ambazo zilionekana kufanya vibaya kitaaluma

Hivyo ni jukumu la kila mdau wa elimu kuiunga mkono serikali katika mpango huu, wa kuinua ubora wa elimu Tanzania, kwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa walimu na kuwahamasisha wazazi wengine kupeleka watoto wao shule ikiwa ni pamoja na kuwahimiza wanafunzi kuhudhuria shuleni bila kutoraka.



Na Ahmed Makongo, Bunda

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Mpango wa Equip wainua kiwango cha elimu
Mpango wa Equip wainua kiwango cha elimu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic22VzttrRwdBksGv1N1YnYlLJsQmXO_ITjvmJDMNSQTcycFt3OiVrSuf-NXVWuDYYajDdK2U2Vv_wRsoHWTALnip5t_XPKL4Jp5aeNJDELXkJtPa90SVfQTXQihPRSxVmldWFhDAQwO0/s640/Elimu.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic22VzttrRwdBksGv1N1YnYlLJsQmXO_ITjvmJDMNSQTcycFt3OiVrSuf-NXVWuDYYajDdK2U2Vv_wRsoHWTALnip5t_XPKL4Jp5aeNJDELXkJtPa90SVfQTXQihPRSxVmldWFhDAQwO0/s72-c/Elimu.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mpango-wa-equip-wainua-kiwango-cha-elimu.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/mpango-wa-equip-wainua-kiwango-cha-elimu.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content