Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Dk. Shein Aanza Ziara Yake Visiwani Zanzibar

RAIS wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameutaka Uongozi wa Mkoa wa Kusini Unguja kutangaza na kuelim...

RAIS wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameutaka Uongozi wa Mkoa wa Kusini Unguja kutangaza na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuenzi  dhana ya  Utalii wa ndani.

Kauli hiyo aliitoa katika majumuisho ya ziara ya Mkoa huo iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA), alisema dhana ya utalii wa ndani ni muhimu kuendelea kutangawa kwani imebeba fursa zitakazoongeza pato la taifa kupitia sekta ya utalii nchini.

Dk. Shein alipongeza  hatua za maendeleo zilizofikiwa na Mkoa huo katika sekta za kilimo, utalii, afya, miundombinu na hatua zilizowekwa za kukabiliana na janga la mabadiliko ya tabia nchi.
 Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na wananchi pamoja na wanachama wa CCM  Jimbo la Mahonda katika uzinduzi wa Tawi la CCM Kitope ‘’B’’ katika ziara yake Zanzibar iliyoanza leo Mkoa wa Kaskazini Unguja.


Kupitia majumuisho  hayo  Dk. Shein  aliwaagiza  Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kujenga utamaduni wa  kutembea vijijini kwa lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya fursa zinazopatikana katika wizara hizo  ili wananchi wazifahamu na kuzichangamkia.

“ Bado kuna wananchi hawajui kama serikali ina mfumo wa uwezeshaji  unatoa mikopo kwa wajasiriamali na vikundi vingine vyenye malengo ya kujikomboa kiuchumi, na hadi hivi sasa tayari zaidi ya bilioni mbili wamekopeshwa wananchi wa maeneo mbali mbali hapa nchini”, alieleza Dk. Shein na kuitaka Wizara ya kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Zanzibar  kutangaza kuwafikia wananchi wa vijijini ili wanufaike na mfuko huo.

Dk. Shein aliwapongeza wakulima wa zao la ndimu ndani ya mkoa huo na kuitaka  Wizara inayohusika na masuala ya kilimo kutumia wataalamu wake  kuwafundishe wananchi mbinu bora za kilimo cha kisasa.

Hata hivyo alisema licha ya Mkoa huo kupata mafanikio mbali mbali bado wanatakiwa kuzidisha bidii katika kudhibiti vitendo vya magendo ya bidhaa mbali mbali vinavyoikosesha serikali mapato.

Dk. Shein ambaye pia ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar  alizindua jengo la Tawi la CCM Kizimkazi Dimbani ndani ya Mkoa huo,  na kuwasihi viongozi wa chama hicho kutumia vikao vya kikatiba wakati wa kufanya maamuzi yanayohusu taasisi hiyo  badala ya kufanya maamuzi binafsi.

Aliwasihi wazee wa CCM kuendeleza utamaduni wa kuwafundisha itikadi vijana ili waweze kujua historia ya chama na nchi ilipotoka kabla na baada ya mapinduzi ya mwaka 1964.

Aliwambia wanachama wa chama hicho na wananchi kwa ujumla kuwa Chama cha Mapinduzi kinapoahidi kinatekeleza kwa wakati kwani miradi yote inayozinduliwa hivi sasa imetokana na usimamizi mzuri wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2016.

Ziara hiyo ya siku mbili katika Mkoa wa Kusini, Dkt. Shein alikagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu katika kijiji cha Kitogani, alitembelea wajasiriamali wa Saccos ya AMCO na kuona mazao wanayozalisha yakiwemo Matikiti maji, mihogo, ndimu na Tungule huko Mtule kijiji cha Paje.


Miradi mingine iliyotembelewa na Dk. Shein ni kukagua mradi wa kisima cha maji safi na salama huko katika mapango ya Mnywambiji pamoja na kuweka jiwe la msingi katika nyumba za kuishi za madaktari wa Vituo vya Afya vya Kajengwa na Muyuni ‘B’  Wilaya ya Kusini Unguja.

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Dk. Shein Aanza Ziara Yake Visiwani Zanzibar
Dk. Shein Aanza Ziara Yake Visiwani Zanzibar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8z20lgbvHxXY69WWn2qQBPf-zdLLyx6UPy94Uc4uOo7gsA2skvJFA_cgFCZluX9SiIHXCAwcGYIaF-3BDPb-VDmOjHAt9xjMl2pPQl7j16a9bxEQo3HDJPcTN0WzOGBIuvC94l-V9EvI/s640/01.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8z20lgbvHxXY69WWn2qQBPf-zdLLyx6UPy94Uc4uOo7gsA2skvJFA_cgFCZluX9SiIHXCAwcGYIaF-3BDPb-VDmOjHAt9xjMl2pPQl7j16a9bxEQo3HDJPcTN0WzOGBIuvC94l-V9EvI/s72-c/01.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/rais-wa-zanzibar-namwenyekiti-wa-baraza.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/rais-wa-zanzibar-namwenyekiti-wa-baraza.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content