Habari Mpya

Monday, 7 August 2017

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo amekabidhi mabati zaidii ya 400 kwa ajili ya kukamilsha ujenzi wa shule za msingi na sekondari,vituo vya afya pamoja na zahanati katika Halmashauri ya Meru ambayo aliahidi wakati wa ziara ya yake wilayani Arumeru mwishoni mwa mwezi  Julai.
Gambo akizungumza mara baada yakukabidhi mabati hayo ambayo yametolewa na kampuni ya China ya ujenzi wa barabara ya Arusha Tengeru,Hanil Jiangsu Joint Venture LTD -amesema hatua hiyo ya kutoa msaada wa mabati ni kuwatia moyo wananchi ili waweze kuchangia shuguli za maenedeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri Happyness Mrisho ameahidi kutumia mabati hayo kama ilivyokusudiwa katika kutekeleza ujenzi wa shule,vituo vya afya na zahanati. 

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -