Habari Mpya

Wednesday, 16 August 2017

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita ,amelishukuru Shirika la Maendeleo la Japani (JICA) kwa kukamilisha mradi wa Barabara na bustani ya Kaburi moja iliyopo mtaa wa Samora jijini hapa.
Meya wa Jiji la Dar es SalaamIsaya Mwita  akiteta jambo na mwakilishi wa JICA Nchini Tanzania Toshio Nagase


Utekelezaji wa mradi huo ulianza mwezi Desemba mwaka jana na kusainiwa na meya huyo na baadae kukabidhiwa kwa halmashauri ya manispaa ya Ilala leo.

Mwita alisema kuwa mradi huo umegharimu jumla ya shilingi milioni 840 ikiwa na malengo ya kuboresha mtaa wa samora ili kuwezesha magari kutembea kwa uangalifu zaidi sambamba na kuliweka jiji kwenye muonekano mzuri.


Alisisitiza kuwa  mradi huo uliochukua nafasi kubwa ya maeneo ya maegesho ya magari, lakini umesababisha kuwa na muonekano mzuri kutokana na maboresho yaliyofanyika.


Wakati huo huo mwakilishi wa JICA Nchini Tanzania Toshio Nagase alieleza kuwa mradi huo utasaidia kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -