Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Wadau warishukuru shirika la Zinduka kukemea vitendo vya ukatili

SERIKALI wilayani Bunda mkoani Mara, imeripongeza shirika lisilokuwa la kiserikali la Zinduka lililoko wilayani humo, linalofadhiliwa na sh...

SERIKALI wilayani Bunda mkoani Mara, imeripongeza shirika lisilokuwa la kiserikali la Zinduka lililoko wilayani humo, linalofadhiliwa na shirika la The Foundation For Civil Society, kwa kuwapatia wananchi elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ili vitendo hivyo viweze kukomeshwa ndani ya jamii.

Pongezi hizo zilitolewa jana na mkuu wa wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili, aliyewakilishwa na katibu tarafa cha Nansimo, Jonas Nyaoja, kwenye mafunzo ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yanayofanyika katika mji mdogo wa Kibara wilayani humo.

Mkuu huyo wa wilaya ya Bunda alisema kuwa serikali wilayani hapa inatambua mchango mkubwa wa shirika hilo katika kutoa elimu juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, ili jamii iweze kupata uelewa na kuachana na vitendo hivyo.
Mkuu wa Wilaya Bunda Lydia Bupilipili .
“Serikali wilayani Bunda inatambua mchango mkubwa unaaotolewa na shirika hili la Zinduka katika kutoa elimu kwa jamii juu ya ukiukwaji haki na unyanyasaji wa kijinsia. Sasa elimu hii wananchi wetu wakiipata itawasaidia kubadilika na kuacha vitendo hivyo” alisema Nyaoja.

Pia, baadhi ya wadau mbalimbali wanaopinga vitendo hivyo wilayani hapa, pia wamelishukuru shirika hilo kwa kuwapatia mafunzo hayo kwa sababu vitendo vya ukatili wa kijinsi vimekithiri sana ndani ya jamii yetu, ukiwemo ukatili wa kiuchumi pamoja na ule wa tendo la ndoa.

Wadau hao ambao ni pamoja na wazee wa mila, wazee maarufu, viongozi wa madhehebu ya dini, vyama vya siasa, watendaji wa vijiji na kata, pamoja na wenyeviti wa vijiji, walisema kuwa Shirika la Zinduka limejikita sanan katika kutoa elimu hiyo kwa jamii.

Waliyaomba mashairika mengine kuiga mfano huo, kwani wananchi wengi wamekuwa wakiendesha vitendo hivyo kwa sababu ya kukosa uelewa na kwamba ni shirika la kwanza kufika mkatika maeneo yao na kuwapatia elimu hiyo.

Walisema kuwa ukatili mwingine ni ubakaji wa wanawake, utumikishaji wa watoto wadogo kwenye shughuli hatarishi ambazo haziendani na umri wao, ukatili wa kutokupeleka watoto shule hususani wa kike, pamoja na unyanyasaji wanawake na wanaume ndani na hata nje ya ndoa.

Waliongeza kuwa ukatili mwingine ufanywa na wanaume kuachia shughuli za kilimo na uzalishaji mali wanawake tu, huku wanaume wengi wakikalia ulevi na uzululaji, ambapo nyakati za chakula ufika majumbani mwao na kudai chakula tena kwa kuamrisha, ambapo wanawake wanaposema hakuna chakula uambulia kichapo au matusi ya uzalilishaji.

Walisema kuwa wamridhika na mafunzo hayo ambayo yamewapatia mwanga, ambapo wataisambaza elimu hiyo katika maeneo yao ili jamii iweze kubadilika.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika la Zinduka, mhasibu wa shirika hilo, Godfrey Anatory, alisema kuwa wanatoa mafunzo hayo kwa makundi mbalimbali ya kijamii katika kata tisa za jimbo la Mwibara na kwamba katika awamu ya kwanza walitoa mafunzo hayo katika kata 13 za majimbo ya Bunda na Bunda mjini.

“Mafunzo haya tunayaendesha kwa kata tisa za jimbo la Mwibara, lakini pia mafunzo kama haya tulikwishayaendesha katika kata 13 za majimbo ya Bunda na Bunda mjini. Na baadaye tuendesha mafunzo haya kwa viongozi mbalimbali wakiwemo maasikari polisi, mahakimu na wanasheria, ili jamii iweze kujua athari za ukatili wa kijinsia na adhabu yake” alisema.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dk. Stanely Maendeka, alisema kuwa malengo ya mafunzo hayo ni kupata uelewa sahihi wa dhana za kijinsia na dhana ya ukatili wa kijinsia, na kupata uelewa na uwezo wa kutetea na kukomesha ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.

Dk. Mahendeka aliyataja maelengo mengine kuwa ni pamoja kurekebisha mapendekezo ya awali ya mradi, ili ibebe shughuli zinazogusa kukomesha ukatili wa kijinsia, kurekebisha bajeti iweze kuingiza au kuchukuwa shughuli zilizopendekezwa, kukomesha ukatili wa kijinsia na kuweza kutekeleza mradi vizuri zaidi na kupata matokeo yaliyotarajiwa.


COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA: Wadau warishukuru shirika la Zinduka kukemea vitendo vya ukatili
Wadau warishukuru shirika la Zinduka kukemea vitendo vya ukatili
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgo4jP-FQwDYqz9gPPq7YAzwS-gywm9hx0hWDqXmj1dIuAX7VJuLf3qN6q4joVLcJpXYsQwFCFEqhHg_RUha6UKH1S9dGzYe2vvw5YpdC0Ta1NVuLsc0_wPP5DME3_nAIo0LAogAqUucAs/s640/Lyidia+Bupili.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgo4jP-FQwDYqz9gPPq7YAzwS-gywm9hx0hWDqXmj1dIuAX7VJuLf3qN6q4joVLcJpXYsQwFCFEqhHg_RUha6UKH1S9dGzYe2vvw5YpdC0Ta1NVuLsc0_wPP5DME3_nAIo0LAogAqUucAs/s72-c/Lyidia+Bupili.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/wadau-warishukuru-shirika-la-zinduka.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/wadau-warishukuru-shirika-la-zinduka.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content