Habari Mpya

Wednesday, 16 August 2017

WAZIRI mkuu Kassim Majaliwa, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Balozi Benedict Mashiba, na kumtaka kuimarisha mahusiano kati ya nchi zote mbili.

Akiongea na balozi huyo akiwa nyumbani kwake Oystabay leo jijini Dar es Salaam, ambapo amemtaka balozi huyo kuhakikisha anaboresha shughuli zote  za Kidiplomasia kati ya Tanzania na Malawi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha anatangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini, ukiwemo mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo nchini hususan katika sekta ya viwanda.
Waziri mkuu Kassim Majaliwa, (kulia) akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini MalawiBenedict Mashiba
Majaliwa amesema licha ya kutangaza fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii pia amemwambia juu ya kuboresha biashara kwa kutumia meli mbili za mizigo za Mv. Ruvuma na Mv. Njombe alizozizindua hivi karibuni.

Amesema kuwa afanye mazungumzo na Watanzania waishio nchini Malawi na kuwasisiza kuishi kwa kuzingatia sheria za nchi husikaikiwa ni pamoja na kuwaunganisha pamoja na kuwashauri waje kuwekeza nchini.


Kwa upande wake Balozi Mashiba amesema atahakikisha anayafanyia kazi maelekezo yote aliyopewa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama pamoja na kuboresha ushirikiano baina ya Tanzania na Malawi.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -