Powered by Blogger.

About

[Michezo kimataifa][column2]

Labels

Blog Archive

Search This Blog

Blog Archive

[random][featured1]

BTemplates.com

MICHEZO KITAIFA

[michezo][column2]

Blogroll

[afya][fbig2]

Contact us

Name

Email *

Message *

BTemplates.com

Na Ahmed Makongo, Bunda: MBUNGE wa Bunda mjini Esther Bulaya, amesema kuwa yeye hana vihoja, jehuri au fujo kama inavyotafasiriwa na ba...

Na Ahmed Makongo, Bunda:

MBUNGE wa Bunda mjini Esther Bulaya, amesema kuwa yeye hana vihoja, jehuri au fujo kama inavyotafasiriwa na baadhi ya watu wasiomtakia mema, baada ya kufungiwa kutokushiriki kwenye vikao vya  Bunge, bali yeye  ni mkweli na mwenye hoja na anayezijua haki zake na kwamba amekuwa akinyimwa haki hizo.
MBunge wa Bunda mjini Esther Bulaya
Mbunge huyo aliyasema hayo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Bunda, mkutano ambao lengo lake  ulikuwa ni kuwaelezea wananchi juu ya ushindi wa kesi ya uchaguzi iliyokuwa imefumguliwa ma wapiga kura wanne wa jimbo hilo, pamoja na kuhusu kufungiwa kushiriki kwenye vikao vya Bunge.
Alisema kuwa yeye kamwe havunji taratibu, bali anazijua haki zake na kwamba kufungiwa  na bunge kwamba ni kwa sababu ya vihoja na vurugu zake kama inavyotafasiriwa na baadhi ya watu si kweli na kuongeza kuwa kilichosababisha kufungiwa ni kile alichokiita ni kusimamia haki zake pamoja na ukweli kwani yeye pia ni waziri kivuli wa Sera, Uratibu na Bunge.
“Mimi pia ni waziri kivuli wa Sera, Uratibu na Bunge, na mimi sina vihoja bali bali ni hoja za msingi, siwezi kukiuka utaratibu maana ninaujua na pia ninatambua haki zangu” alisema.
Alisema kuwa kuhusu kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo hilo, amemshinda mara tano mfululizo mpinzani wake Stephen Wassira, pamoja na wapiga kura wanne, waliokuwa wamefungua kesi hiyo, baada ya mahakama ya rufaa hivi karibuni kutupilia mbali rufaa iliyokuwa imekatwa na wapiga kura hao, baada ya kushindwa katika mahakama kuu kanda ya Mwanza mjini Musoma.
Hata hivyo, alisema kuwa amekuja kuwauliza wapiga kura ambao ndio waajiri wake kama wanamruhusu afunguwe kesi ya madai dhidi ya wapiga kura hao, ambao walishindwa katika kesi hiyo ili waweze kulipa gharama zote za kesi hiyo, ambapo wananchi hao walisikika wakisema kwa sauti kuwa fungua kesi wakulipe.
Alisema kuwa atawasiliana na mwanasheria wake Tundu Lissu ili waweze kufungua kesi hiyo ya madai kwani katika hukumu, mahakama ya rufaa ilisema kuwa warudishe gharama za zote za kesi hiyo.
Alisema kuwa hilo litakuwa fundisho kwa watu wengine kuacha kupotezea muda watu bure pasipo sababu za msingi, wakati wakijua fika kuwa alishinda katika uchaguzi huo wa mwaka 2015 kihalali kabisa.
Alisema kuwa wananchi wa jimbo lake amewamisi kwa kukosa mawasiliano na kupata maoni, changamoto na matatizo yao kwa kipindi chote cha miaka miwili, ambacho alikuwa akishughulikia kesi, wakati jimbo lake lina changamoto nyingi zikiwemo za maji, na wanyama waharibu kutoka katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kushambulia mazao ya wakulima.
“Niliwamisi sana eti na nyinyi mumenimisi si ndiyo” alisema huku akishangiliwa na kuitikiwa na wananchi kwamba walimumisi kwa kipindi kirefu.
Katika hatua nyingine pia mbunge huyo alisema kuwa kutokana na hali ya maji katika mji wa Bunda,  kuwa ya kusuasua, sasa atatoa kiasi cha shilingi milioni 20 kutoka kwenye mfuko wa jimbo, na kununua mabomba kwa ajili ya kuunganisha maji katika kata zote za mji huo, ambapo pia amewataka wananchi kutokulazimishwa kununua vifaa vya maji katika duka la mtumishi mmoja wa mamlaka ya maji kama waziri mwenye dhamana alivyokwishaagiza.
Pia, alisema kuwa pia atahakikisha inapatikana gari nyingine ya kituo cha polisi Bunda kwa ajili ya kufanyia doria na kupambana na uharifu na vitendo vya uharifu, ambapo amewataka wananchi jimboni humo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa askari polisi ili waweze kutekeleza wajibu wao ipasavyo ya kulinda raia pamoja na mali zao.
Alisistiza kuwa yeye ni mbunge wa vitendo lazima ahakikishe jimbo hilo linakuwa na maendeleo.
Mkutano huoambao ulihudhuriwa na maelefu ya wananchi, pia walikuwepo viongozi mbalimbali wa chama hicho, wakiwemo wabunge pamoja na Naibu katibu mkuu wa Chadema Salumu Mwalimu.

COMMENTS

[facebook]
Name

AFYA,6,GURUDUMU LA MAISHA,2,HABARI,48,KIJIJINI,7,KIMATAIFA,9,MAHUSIANO NA SAIKOLOJIA,2,MAKALA,2,MAKALA YA ELIMU,1,MICHEZO,2,MIKOANI,4,SARAFU,4,VIDEO,4,ZANZIBAR,1,
ltr
item
LENZI MEDIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhH1Hl9rFVCFBX547CTc2Bz7IQR0wHr3Q9APlMEwtk8f-D5IG3xgsoOYh95acpjDVAvz0WuimfycTE7ZRp5NuVxyXvYtV1YCF-aHvlqIQ25HZwj0qCEgjFAYCoGbovuyoCMopGRtutt7Fk/s640/Bulaya.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhH1Hl9rFVCFBX547CTc2Bz7IQR0wHr3Q9APlMEwtk8f-D5IG3xgsoOYh95acpjDVAvz0WuimfycTE7ZRp5NuVxyXvYtV1YCF-aHvlqIQ25HZwj0qCEgjFAYCoGbovuyoCMopGRtutt7Fk/s72-c/Bulaya.jpg
LENZI MEDIA
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/na-ahmed-makongo-bunda-mbunge-wa-bunda.html
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/
https://lenzimedia.blogspot.com/2017/08/na-ahmed-makongo-bunda-mbunge-wa-bunda.html
true
2372332392983471599
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content