Habari Mpya

Tuesday, 15 August 2017

WAZIRI mkuu Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa mkoani Tabora kuacha kuwatumia watoto kama vibarua kwenye mashamba ya tumbaku bali wawapeleke shule.
Alitoa agizo hilo Jumapili, Agosti 13, 2017 alipokuwa annazungumza na watumishi idara za kilimo na ushirika na viongozi wa wilaya ya mkoa huo kwenye kikao alichokiitisha ili kwa ajili ya kuwapa maagizo.
Waziri mkuu Kasim Majaliwa akisisitiza jambo wakati anaongea na viongozi wa mkoa wa Tabora

“Ninasisitiza jamii iwapeleke watoto shule kuanzia elimu ya awali hadi sekondari na tuache kuwatumia watoto wadogo kama vibarua kwenye mashamba ya tumbaku. Wakuu wa wilaya simamieni eneo hili la kuondoa watoto kwenye ajira,” alisema.
Wakati huo huo Majaliwa aliwataka viongozi hao kusimamia elimu ya mtoto wa kike na kuhakikisha kuwa wanawalinda kuazia elimu ya msingi na sekondari hatimaye wanapofikia ngazi ya chuo kikuu watakuwa wamepevuka na na kujilinda wenewe.

Akihutubia kwenye mikutano ya hadhara wakati wa ziara yake ya siku nne, aliwaasa vijana wa kiume wasithubutu kuwaoa mabinti wanaosoma, kwani kwa kufanya hivyo, wataishia kufungwa jela miaka 30.
Waziri mkuu akiongea na viongozi wa mkoa wa Tabora

Katika ziara hiyo aliwaonya wazazi wanaoamua kuwaoza mabinti zao ili wapate mahari, na na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo wako katika hatari ya kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 endapo watabainika kushirikiana na waoaji.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -