Habari Mpya

Tuesday, 29 November 2022

 

KKATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja ambaye hakufahamika kwa jina Amenusurika na kipigo na wananchi Wenye hasira kali mara baada ya kufanya Uharibifu kwa kuharibu mashine ya Kusaga mahindi ya Mjasiliamali mwenzake kutokana na wivu wa kimaendeleo.



Kijana huyo mkazi wa kijiji cha Nyikonga wilayani Mbogwe Mkoani Geita amenusurika na kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali mara baada ya kuvamia nyakati za usiku na kuanza kuharibu mashine ya kusaga mahindi iliyo jirani yake inayotumia mafuta ambapo yeye ameajiriwa katika mashine inayotumia Umeme.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Mperwa Sekela amesema kesi hiyo kwa sasa iko mahakamani huku  akitoa wito kwa wananchi kuachana na vitendo vya kujichulia sheria mkononi.

Kwa upande wake mmiliki wa mashine hiyo iliyoharibiwa hakuwa tayari kuzungumzia tukio hilo huku mmiliki wa mashine alikokuwa anafanyia kazi kijana aliefanya uharibifu huo amekiri kutokuwa na ugomvi wowote na jirani yake huku baadhi ya wananchi wakishangazwa na kitendo alichokifanya kijana huyo.

Mpaka sasa kijana huyo yuko chini ya uangalizi wa vyombo vya  Dola katika hatua zaidi za uchunguzi wa Tukio alilofanya.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -