Habari Zote
Archive for August 2022
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amewakumbusha wananchi wa kijiji cha Vuchamangofi wanaohitaji kuwekewa umeme gharama zake ni Sh. 27,000 kwa vna sio vinginevyo kama ambavyo wamekuwa wakidanganywa
"Msikubali kutozwa
zaidi ya Sh.27,000 kwa sasa umeme sio hanasa, kila mtu anatakiwa kupata huduma
hii kwa gharama ya chini kwa sababu serikali imeamua kutoa huduma hii maeneo
yote nchini," amesisitiza Chongolo.
Chongolo ameyasema hayo
akiwa wilani Mwanga mkoani Kilimanjaro akiwa kwenye mwendelezo wa ziara ya
siku tano ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, miradi ya maendeleo na
kuhimiza sensa ya watu na makazi
Amesema kuna watendaji
wasio waaminifu wanawalaghai wananchi kulipa zaidi ya kiasi hicho.
Rais wa Tanzania, Samia
Suluhu Hassan ameteua maofisa 22 kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Kwa mujibu wataarifa iliyotolewa
usiku wa Jumamosi, Agosti 6, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, Zuhura Yunus amefanya uteuzi huo juzi Alhamisi Agosti 4, 2022.
Miongoni mwa
walioteuliwa kuwa majaji wa Mahakama Kuu ni pamoja na Gabriel Pascal Malata
ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Wakili Mkuu wa Serikali na aliyekuwa Msajili
wa Mahakama ya Rufani, Kevin Mhina.
Majaji hao walioteuliwa
ambao tarehe ya kuapishwa itatangazwa ni;
1. Kevin David Mhina-
kabla ya uteuzi alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani
2. Gabriel Pascal
Malata-kabla ya uteuzi huu alikuwa Wakili Mkuu wa Serikali
3. Adrian Philbert
Kilimi- kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili Mahakama
4. Happiness Philemon
Ndesamburo- kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama;
5. Victoria Mlonganile
Nongwa- kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama
6. Obadia Festo
Bwegoge- kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama
7. Ruth Betwel
Massam-kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama
8. Godfrey Ntemi
Isaya-kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama
9. Gladys Nancy
Barthy-kabla ya uteuzi alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama
10. Haji Suleiman Haji-
kabla ya uteuzi alikuwa Mwendesha Mashitaka Mfawidhi Mahakama Kuu, Zanzibar
11. Fatma Rashid
Khalfan-kabla ya uteuzi alikuwa Kamishna Tume ya Haki za Binadamu na Utawala
Bora
12. Abubakar A.
Mrisha-kabla ya uteuzi alikuwa Wakili wa Serikali
13. Lusungu Hemed
Hongoli-kabla ya uteuzi alikuwa Wakili Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali
14. Monica Peter
Otaru-kabla ya uteuzi alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali
15. Kamana Stanley
Kamana-kabla ya uteuzi alikuwa Mkurugenzi Msaidizi (Tamisemi)
16. Hamidu Rajabu Mwanga-kabla ya uteuzi
alikuwa Mkurugenzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi
17. Marlin Leonce
Komba-kabla ya uteuzi alikuwa Mkurugenzi wa Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi
18. Dk Mwajuma Kadilu
Juma-kabla ya uteuzi alikuwa Mhadhiri Msaidizi, Chuo Kikuu Mzumbe
19. Dk Cleophas K.K.
Morris-kabla ya uteuzi alikuwa Mhadhiri, Chuo Kikuu Dar es Salaam
20. Asina A.
Omani-kabla ya uteuzi alikuwa Mhadhiri, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ni
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
21. Aisha Zumo Bade-
kabla ya uteuzi alikuwa Wakili wa Kujitegemea
22. Mussa Kassim
Pomo-kabla ya uteuzi alikuwa Wakili wa Kujitegemea.
Taarifa hiyo imesema
kuwa tarehe ya kuapishwa majaji hao wateule itatangazwa baaadaaye.
RAIS wa Tanzania, Samia
Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kuboresha huduma za afya na maji
katika maeneo mbalimbali nchini.
Amesema anatambua
matatizo yanayowakabili kina mama kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo
muhimu hivyo Serikali itahahakikisha mpaka kufikia mwaka 2025 tatizo la maji
nchini linakuwa limekwisha.
Rais Samia Suluhu Hassan akizindua mradi wa maji wa Makongolosi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.
Rais Samia ameyasema
hayo leo wakati akizindua mradi wa maji katika kata ya Makongorosi Wilaya ya
Chunya wenye thamani ya Sh2.5 bilioni utakaozalisha maji lita Milioni mbili kwa
siku.
Amesema katika ilani ya
uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ifikapo 2025 ilielekeza kutatua tatizo la
maji na kwa Mkoa wa Mbeya kuna miradi 50 ambayo imefikia asilimia 95 na ifikapo
2025 tatizo la maji litakwisha kwa asilimia 100.
Kwa upande wake, Katibu
Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Athon Sanga amesema mradi huo umefikia asilimia
70 ambao utazalisha lita milioni mbili zitakazo ondoa tatizo la maji katika
Wilaya ua Chunya.
Amesema wizara ina
mpango wa kuchimba visima vikubwa vya maji
katika mji wa Makongorosi ili kuondokana na hadha kwa baadhi ya maeneo
huku akimpongeza Mbunge wa Lupa, Masache
Kasaka kwa kutatua changamoto ya maji jimboni kwake kwa kuchimba visima.
Kwa upande wake, Mbunge
Kasaka amemuomba Rais Samia kusaidia kuboreshwa miundombinu ya barabara kutoka
chunya mpaka kijiji cha Itumbi ambako kuna shughuli za uchimbaji wa madini ili
kufungua fursa za kiuchumi.
Mchimbaji mdogo wa Madini
Kata ya Matundasi, Aden Mwakyusa amesema ujio wa Rais Samia ikawe chachu ya
changamoto za wachimbaji madini kutatuliwa pamoja na kuhodhi maeneo ambayo
yanashikiliwa na wachimbaji wakubwa.
CHANZO MWANANCHI
WAZIRI mkuu wa
Tanzania KASSIM MAJALIWA amezindua mradi unaofahamika kama farm clinic wenye
lengo la kuwezeshwa wakulima kufikia ajenda ya 10/30 yenye kauli mbiu ya kilimo
ni biashara kupitia farm clinic.
MAJALIWA amefanya
uzinduzi huo alipo tembelea maonesho ya nane nane jijini Mbeya huku akiwahimiza
vijana kuingia kwenye sekta ya kilimo kwa kuwa serikali imeandaa mipango mingi
na mizuri kwa ajiri yao.
![]() |
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa |
MAJALIWA amesema
kuwa anaomba kila mwananchi ajishughulishe na shughuli ambayo itamleta uchumi
ambayo itamsaidia kupata kipato ambacho kitamsaidia kila mtanzania kuendesha
familia.
Kwa upande wake
mbunge wa jimbo la mbeya mjini na spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa
Tanzania TULIA ACKSONI MWANSASU ametumia nafasi hiyo hiyo kumshukuru rais samia
suruhu hassani kwa kuleta mradi mkubwa wa maji ambao unaenda kumaliza
changamoto ya maji jijini Mbeya.
NA: ANYIGULILE
ZAKARIA
SERIKALI ya kijiji
cha Lulembela wilayani Mbogwe Mkoani Geita imewatahadharisha baadhi ya watu
wenye tabia ya kuwaficha watoto kisha kuanza kudai fidia kwa wazazi wao kwa
kisingizio walikuwa wamepotea.
Kaimu Afisa
Mtendaji Wa kijiji hicho PAUL NTAHENGAMA ametoa tahadhari kwa watu wenye tabia
hiyo nakwamba wamekuwa wakipata taarifa kutoka kwa wananchi japo hawajabaini
juu ya uwepo wa vitendo hivyo kwani wengi wanaowakota watoto hao huwaokota kwa
nia njema na si kwa biashara.
kwa mujibu wa
maelezo ya wananchi katika Eneo hilo wamedai wimbi la kupotea watoto kwa sasa
ni kubwa nakwamba cha kushangaza pindi wanapowapata watoto hao huwalazimu kutoa
fidia kuwakomboa kutoka kwa wasamalia wema waliowaokota jambo Ambalo wamehisi
huenda kuna biashara ambayo inaendelea. Moja kati ya mzazi ambae amekumbana na
changamoto ya mtoto wake kupotea nakulipishwa fidia amesema.
Mwenyekiti wa
serikali ya kijiji hicho MAISHA WILLIAM MAGINYA amesema Uvumi wa kuwepo kwa
kikundi cha watu wanaotumia Fursa hiyo ya kuficha watoto kujiingizia kipato wameendelea kulifanyia kazi ili kubaini
uwepo wa vitendo hivyo.
Katika hatua
Nyingine Bw William amewataka wazazi na walezi kuwa waangalifu kwa watoto wao
ili kuondokana na changamoto kama hizo kwakuwa wazazi wengi wamekuwa bize na
uzalishaji mali nakusahau malezi kwa watoto.
NA NICHORAS PAUL LYANKANDO
BAADHI ya wafanyabiashara katika mamlaka ya mji mdogo wa katoro wilayani geita mkoani Geita wamesema sheria kandamizi za ulipaji wa kodi imekuwa kisababishi cha wengi wao kuingia katika vishawishi vya utoaji wa rushwa ili kuendelea na biashara.
Wakizungumza
katika moja ya kikao na maafisa wa Mamlaka ya Mapato TRA Wafanyabiashara hao
wametoa malalamiko yao juu Sheria kandamizi Ambazo zinawakandamiza
wafanyabiashara.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara CHARLES MAKANJI amesema TRA wamegeuka
kuwa chanzo cha kuwadidimiza wafanyabiashara kwa kuwatoza faini Ambazo
haziendani na mitaji yao.
Akitoa
Ufafanuzi wa suala la kodi Mwalimu Toa Elimu ya Kodi kanda ya ziwa LUTUFYA
MTAFYA amesema wao wanasimamia Sheria na Hawamkandamizi mfanyabiashara hivyo
amewaomba wawasilishe kero zao katika Ofisi za mamlaka hiyo na kero zao
kutatuliwa haraka iwezekenavyo.
Katika
Hatua nyingine akawaomba kutoziogopa Ofisi za TRA badala yake watumie ofisi hizo
kama kimbilio la kwanza kutatuliwa kero zao.
NA
NICHORAS PAUL LYANKANDO