Habari Mpya

Saturday, 6 August 2022

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amewakumbusha wananchi wa kijiji cha Vuchamangofi wanaohitaji kuwekewa umeme gharama zake ni Sh. 27,000 kwa vna sio vinginevyo kama ambavyo wamekuwa wakidanganywa


"Msikubali kutozwa zaidi ya Sh.27,000 kwa sasa umeme sio hanasa, kila mtu anatakiwa kupata huduma hii kwa gharama ya chini kwa sababu serikali imeamua kutoa huduma hii maeneo yote nchini," amesisitiza Chongolo.

Chongolo ameyasema hayo akiwa wilani Mwanga mkoani Kilimanjaro akiwa kwenye mwendelezo wa ziara ya siku tano ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, miradi ya maendeleo na kuhimiza sensa ya watu na makazi

Amesema kuna watendaji wasio waaminifu wanawalaghai wananchi kulipa zaidi ya kiasi hicho.



Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -