Habari Mpya

Thursday, 4 August 2022

BAADHI ya wafanyabiashara katika mamlaka ya mji mdogo wa katoro wilayani geita  mkoani Geita wamesema sheria kandamizi za ulipaji wa kodi imekuwa kisababishi cha wengi wao kuingia katika vishawishi vya utoaji wa rushwa ili kuendelea na biashara.

Wakizungumza katika moja ya kikao na maafisa wa Mamlaka ya Mapato TRA Wafanyabiashara hao wametoa malalamiko yao juu Sheria kandamizi Ambazo zinawakandamiza wafanyabiashara.



Kwa upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara CHARLES MAKANJI amesema TRA wamegeuka kuwa chanzo cha kuwadidimiza wafanyabiashara kwa kuwatoza faini Ambazo haziendani na mitaji yao.

Akitoa Ufafanuzi wa suala la kodi Mwalimu Toa Elimu ya Kodi kanda ya ziwa LUTUFYA MTAFYA amesema wao wanasimamia Sheria na Hawamkandamizi mfanyabiashara hivyo amewaomba wawasilishe kero zao katika Ofisi za mamlaka hiyo na kero zao kutatuliwa haraka iwezekenavyo.

Katika Hatua nyingine akawaomba kutoziogopa Ofisi za TRA badala yake watumie ofisi hizo kama kimbilio la kwanza kutatuliwa kero zao.

NA NICHORAS PAUL LYANKANDO


Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -