Habari Mpya

Thursday, 4 August 2022

 

WAZIRI mkuu wa Tanzania KASSIM MAJALIWA amezindua mradi unaofahamika kama farm clinic wenye lengo la kuwezeshwa wakulima kufikia ajenda ya 10/30 yenye kauli mbiu ya kilimo ni biashara kupitia farm clinic.

MAJALIWA amefanya uzinduzi huo alipo tembelea maonesho ya nane nane jijini Mbeya huku akiwahimiza vijana kuingia kwenye sekta ya kilimo kwa kuwa serikali imeandaa mipango mingi na mizuri kwa ajiri yao.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa


MAJALIWA amesema kuwa anaomba kila mwananchi ajishughulishe na shughuli ambayo itamleta uchumi ambayo itamsaidia kupata kipato ambacho kitamsaidia kila mtanzania kuendesha familia.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la mbeya mjini na spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania TULIA ACKSONI MWANSASU ametumia nafasi hiyo hiyo kumshukuru rais samia suruhu hassani kwa kuleta mradi mkubwa wa maji ambao unaenda kumaliza changamoto ya maji jijini Mbeya.

NA: ANYIGULILE ZAKARIA


Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -