Habari Zote
Archive for October 2017
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amekagua eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya na yakisasa itakayotoa huduma za usafirishaji katika Ziwa Victoria.
Akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Prof. Mbarawa, amewataka wafanyakazi wa Kampuni hiyo kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi ili kazi hiyo ianze mara moja na kukamilika kwa wakati.
“Mkandarasi ameshapatikana hivyo hakikisheni mnatoa ushirikiano na mnafanya uhakiki wa kimahesabu vizuri ili kazi hii ifanyike kwa gharama nafuu, ubora na muda mfupi”, amesema Prof. Mbarawa.
Katika hatua nyingine, Waziri Mbarawa, amekagua maendeleo ya ukarabati wa meli ya Mv. Clarias na Mv. Umoja ambapo ameeleza kuridhishwa kwake na hatua zilizofikiwa, na hivyo kuwataka MSCL kutafuta mizigo ya kusafirisha kutoka Bandari ya Mwanza kwenda Bandari ya “Port Bell”, nchini Uganda.
“Kukamilika kwa meli kuwiane na kasi ya kutafuta mzigo mwingi ili meli hizi zifanye biashara wakati wote na kuhakikisha Kampuni yenu inapata mapato mengi yatakayowawezesha kujiendesha kwa faida”, amesisitiza Waziri Mbarawa
Naye, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Erick Hamissi, amemhakikishia Prof. Mbarawa, kuwa wamejipanga kufanya ukarabati mkubwa wa meli za Mv. Victoria, Butiama na Liemba ili kuziwezesha meli hizo kufanya kazi katika ubora wake wa awali na kupunguza tatizo la usafiri katika ziwa Victoria na Tanganyika.
“Tumeweka mkakati wa kuhakikisha tunazikarabati meli zetu zote ili ziwe katika ubora unaostahili wakati wote”, amefafanua Bw. Hamissi.
Katika kuhakikisha maendeleo ya kibiashara na kuichumi yanafikiwa katika Ukanda wa maziwa makuu nchini, Serikali imejipanga kuhakikisha inafufua usafiri wa meli za abiri na mizigo katika ukanda huo.
Akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Prof. Mbarawa, amewataka wafanyakazi wa Kampuni hiyo kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi ili kazi hiyo ianze mara moja na kukamilika kwa wakati.
“Mkandarasi ameshapatikana hivyo hakikisheni mnatoa ushirikiano na mnafanya uhakiki wa kimahesabu vizuri ili kazi hii ifanyike kwa gharama nafuu, ubora na muda mfupi”, amesema Prof. Mbarawa.
Katika hatua nyingine, Waziri Mbarawa, amekagua maendeleo ya ukarabati wa meli ya Mv. Clarias na Mv. Umoja ambapo ameeleza kuridhishwa kwake na hatua zilizofikiwa, na hivyo kuwataka MSCL kutafuta mizigo ya kusafirisha kutoka Bandari ya Mwanza kwenda Bandari ya “Port Bell”, nchini Uganda.
“Kukamilika kwa meli kuwiane na kasi ya kutafuta mzigo mwingi ili meli hizi zifanye biashara wakati wote na kuhakikisha Kampuni yenu inapata mapato mengi yatakayowawezesha kujiendesha kwa faida”, amesisitiza Waziri Mbarawa
Naye, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Erick Hamissi, amemhakikishia Prof. Mbarawa, kuwa wamejipanga kufanya ukarabati mkubwa wa meli za Mv. Victoria, Butiama na Liemba ili kuziwezesha meli hizo kufanya kazi katika ubora wake wa awali na kupunguza tatizo la usafiri katika ziwa Victoria na Tanganyika.
“Tumeweka mkakati wa kuhakikisha tunazikarabati meli zetu zote ili ziwe katika ubora unaostahili wakati wote”, amefafanua Bw. Hamissi.
Katika kuhakikisha maendeleo ya kibiashara na kuichumi yanafikiwa katika Ukanda wa maziwa makuu nchini, Serikali imejipanga kuhakikisha inafufua usafiri wa meli za abiri na mizigo katika ukanda huo.
TUME ya uchaguzi imeahirisha uchaguzi katika kaunti za Kisumu,
Siaya, Migori na Homa Bay.
Vituo vya kura katika baadhi ya maeneo tayari
vimefungwa.
Kinyume na uchaguzi wa mwezi Agosti, katika
vituo vya kupigia kura hakukuwa na foleni ndefu.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga amesusia
uchaguzi huo na kuwataka wafuasi wake wasalie manyumbani
Uchaguzi huu unatokana na hatua ya Mahakama ya
Juu kufuta uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti
HOSPITALI ya rufaa ya mkoa wa Tanga, Bombo,
haina chumba cha kuwalaza wagonjwa mahututi (ICU) hali inayosababisha wagonjwa
wanaohitaji uangalizi wa matibabu, hulazimsihwa kuwekwa katika wodi za wagonjwa
wengine, wakiwa na mitungi ya mashine za gesi za kupumulia.
Uchunguzi uliofanywa na Majira takribani mwezi
mmoja katika hospitali hiyo ya rufaa inayopokea wagonjwa kutoka katika vituo
vya afya na hospitali za wilaya nane zilizopo mkoani hapa, na kuthibitishwa na
Katibu Tawala wa mkoa wa Tanga (RAS) Injinia Zenna Said, Mganga Mkuu wa mkoa wa
Tanga, Dk. Asha Mahita na Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dk. Jumanne Karia
kwa pamoja walielezea jitihada za mkoa za kuhakikisha wanajenga chumba hicho.
Hospitali hiyo kongwe hapa nchini, imekuwa na
tatizo hilo takribani miaka 7 sasa, kwa chumba hicho kukosekana ambapo awali
walikuwa wakitumia chumba kimoja kabla ya kusitisha kualza wagonjwa, kikawa
kinatumiwa na watoto wadogo lakini baadaye kikawa kinatumiwa na wagonjwa
wanaotumia kadi za huduma ya Bima ya Afya, lakini sasa kinatumika kwa shughuli
nyingine za hospitali.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Tanga, wamekuwa
wakilalamikia hali hiyo wakieleza kwamba wagonjwa Mahututi kuwachanganya na
wagonjwa wengine huku wakiwa na mitungi ya gesi ni kutowatendea haki, kwa kuwa
wanaporuhusiwa ndugu kuona wagonjwa kunakuwa na msongamano mkubwa na kelele za
hapa na pale za kufariji wagonjwa wengine.
“Nilishtuka nilipoingia wodi ya Galanosi kule
kwa akina mama nilimkuta mke wa diwani wa Kirare, Saleh Mwagilo akiwa amewekewa
mashine ya gesi huku akiwa mahututi, nilishangaa nilipouliza nikaambiwa
hospitali haina chumba cha wagonjwa mahututi,” alisema Haruna Magembe aliyekuwa
na mgonjwa katika wodi hiyo ya Galanosi.
Alisema kuwa licha ya kuwepo mgonjwa huyo katika
wodi nyingine mbalimbali zimekuwa na wagonjwa mahututi wengi wanaochanganywa na
wagonjwa wa kawaida haliambayo imekuwa ikileta tafsiri mbaya ya suala la
viongozi wa mkoa kuwajibika katika kuhakikisha chumba hicho kinapatikana ili
kuwawezesha wagonjwa hao kupata tiba stahili kwa mujibu wa taratibu na sera ya
wizara ya afya.
Alipotafutwa diwani huyo kwa ajili ya kuelezea
suala la mgonjwa wake huyo, hakuweza kupatikana lakini mtu wake wa karibu
aliyejitambulisha kwa jina la Kasirani kasirani, alisema amemhamishia mkewe
huyo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako anaendelea na matibabu baada
ya kulazwa takribani wiki mbili akiwa na mtungi wa oksijeni bila mafanikio.
Alipoulizwa kuhusu hali hiyo Katibu Tawala wa
mkoa wa Tanga, Injinia Zena alikiri kukosekana kwa chumba hicho, lakini alisema
kwa taarifa za jitihada zinazofanyika kupata chumba hicho, alimwelekeza
mwandishi wa habari hizi akakutane na Mganga Mkuu wa mkoa Mahita ambaye atakuwa
na majibu kuhusu kukosekana kwa ICU katika hospitali hiyo.
“Ni kweli lakini sisi kama mkoa tumekuwa na
mipango mbalimbali ya kupatikana lakini nenda kwa Mganga Mkuu atakupa tumefikia
wapi kuhusu kupatikana kwa ICU,” alisema Injinia Zenna.
Dk. Mahita alipoulizwa kuhusu suala hilo,
alisema kuwa ni kweli hawana ICU katika hospitali hiyo lakini wagonjwa wenye
mahitaji hayo wamekuwa wakiwahudumia vizuri licha ya kukosa chumba kinachofaa
kwa huduma hiyo na kwamba hawawezi kuwazuia watu wanaokuja kuwaona wagonjwa
waliowachanganya na wagonjwa wengine.
Hata hivyo, Dk Mahita ambaye alisema pamoja na
kukosa huduma hiyo hospitali hiyo katika kipindi cha hivi karibuni wameweza
kuboresha huduma mbalimbali na kuhusu ICU wamekuwa na jitihada mbalimbali za
kuhakikisha wanamaliza tatizo hilo baada ya kuomba mkopo kwa Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya (NHIF).
“Tumeomba mkopo NHIF kwa ajili ya ICU, lakini
kwa sasa wagonjwa wanaokuja kwa mahitaji ya huduma ya ICU tunawapa huduma,
tunachokosa ni eneo la kutolea huduma hiyo tu,” alisema na kuongeza “Hatuwezi
kuwazuia watu wasiende kutazama wagonjwa wao waliokuwa na oksijeni, lakini
ukitaka taarifa zaidi nenda kamuone Dk. Karia ambaye ni Mganga Mfawidhi wa
hospitali, atakupa hadi sasa tumefikia wapi katika suala hilo,”.
Akizungumzia kuhusu hali hiyo Mganga Mfawidhi wa
hospitali hiyo, Dk. Karia alisema kuwa ni kweli chumba hicho kwa sasa hakipo
katika hospitali hiyo baada ya chumba kilichokuwa kikitumika zamani hakina
mfumo wa kutumia gesi pamoja na vifaa vya ICU, hivyo wakaamua kuwachanganya
wagonjwa wenye mahitaji hayo na wagonjwa wengine, lakini tangu mwaka 2013
wameanza ukarabati wa jengo ambalo litatumika kwa huduma hiyo.
Alisema chumba wanachokifanyia ukarabati sasa
ili kitumike kuwa ICU ni kile kilichokuwa kikitumika kama chumba cha Upasuaji
(Theatre) baada ya mradi wa KfW kutoa fedha za ujenzi wa chumba cha Upasuaji
kipya kinachotumika sasa na kwamba sasa wanaendelea kutafuta fedha ili waweze
kukamilisha katika kipindi kifupi kijacho.
“Ni kweli kile chumba cha mwanzo kilichokuwa
kikitumika kama ICU hatukitumii tena na tunachanganya wagonjwa huko katika
mawodi, lakini chumba kile kilikuwa hakina mfumo wa gesi, pia hakikuwa na vifaa
vinavyohitajika kwa wagonjwa mahututi ikiwemo vitanda,” alisema Dkt Karia.
Aliongeza kusema kwamba katika bajeti yam waka
2017/2018 itatumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ICU na kiasi cha shilingi
milioni 231 ilitengwa mwaka 2016/2017 kwa jili ya kutengeneza mfumo wa gesi
katika chumba hicho ambapo hospitali kwa kushirikiana na ofisi ya Katibu
Tawala, imeanza kushughulikia suala hilo la gesi ambayo pia wataiuza katika
hospitali nyingine baada ya kuanza kazi.
“Vile vile kuna vifaa vya msaada kutoka nchini
Ujerumani Mwenyekiti wetu wa bodi ya Hospitali Zahra Noor kwa kushirikiana na
kaka yake Habib Noor na baadhi ya wafanyabiashara wa hapa Tanga akiwemo
Selemani Rahaleo, watasaidia hiyo ICU yetu ikianza kazi,” alisema Dkt Karia na
kuongeza kwamba wameomba mkopo wa kiasi cha shilingi milioni 560 kutoka NHIF.
Akizungumza na gazeti hili Meneja wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afy (NHIF) mkoani Tanga, Ali Mwakababu alisema ni kweli
hospitali hiyo imeomba mkopo wa kiasi cha shilingi milioni 560 kwa ajili ya
ukarabati wa wodi ya akina mama na watoto pamoja na chumba cha magonjwa mahututi
(ICU).
SERIKALI inatarajia
kuajiri wafanyakazi 400 wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi
kifupi kijacho ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika
Mamlaka hayo, hatua inayotarajiwa kuongeza ufanisi na makusanyo ya kodi.
Naibu Waziri wa Fedha
na Mipango Dk. Ashatu Kijaji (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na
watumishi wengine wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Shinyanga,
alipofanya ziara ya kikazi kukagua namna Mamlaka hayo inavyokusanya kodi.
Naibu Waziri wa Fedha
na Mipango Dk. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto) akizungumza na baadhi ya Viongozi
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Shinyanga kuhusu kufanya juhudi ya
kukusanya mapato ili azma ya Serikali ya kuwahudumia wananchi kikamilifu
itimie.
Ahadi hiyo imetolewa
Mjini Shinyanga na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji, alipokuwa
akizungumza na viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wakati wa
ziara yake ya kikazi ya kukagua utendaji wa Mamlaka hayo mkoani humo.
Dk. Kijaji amesema
kuwa taratibu zote zimekamilika na wakati wowote nafasi za ajira zitatangazwa
na kwamba nafasi hizo zimelenga kuiwezesha TRA kuwafikia watu wengi zaidi na
kuongeza wigo wa makusanyo ya kodi.
Naibu Waziri wa Fedha
na Mipango Dk. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto) akizungumza na baadhi ya Viongozi
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Shinyanga kuhusu kufanya juhudi ya
kukusanya mapato ili azma ya Serikali ya kuwahudumia wananchi kikamilifu
itimie.
“Tunatambua changamoto
ya uchache wa watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ndio maana tumeamua
kuajiri wafanyakazi hao 400 ambao ni wengi kuliko kada nyingine ili tuweze
kuimarisha utendajikazi wa Mamlaka na hivyo kuongeza makusanyo ya kodi
zinazotakiwa kwa shughuli za maendeleo nchini” alisema .
Alisema kuwa pamoja na
uhaba wa watumishi, anaamini kuwa lengo la mwaka huu la kukusanya shilingi
trilioni 17 ambazo Mamlaka hayo imepangiwa yatafikiwa na ikiwezekana kuzidi kwa
kutumia wafanyakazi waliopo.
Dk. Kijaji alitoa rai
kwa wafanyakazi wa TRA kuwa waadilifu na kwamba atakayebainika kukiuka maadili
yake ya kazi atachukuliwa hatua kali za kinidhamu na kisheria.
Awali Meneja wa
Mamlaka ya Mapato mkoa wa Shinyanga Jumbe Samson, alieleza kuwa mkoa wake
umepangiwa lengo la kukusanya Shilingi bilioni 18 na kwamba wanauhakika wa
kufikia lengo hilo kutokana na mikakati mbalimbali waliyojipangia ikiwemo
kusimamia ukusanyaji kodi kikamilifu katika sekta ya madini.
Kwa upande wake, Kaimu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Beatus Nchota alisema kuwa
Mamlaka yake imejiwekea mipango ya kufungua ofisi zake kila wilaya hapa nchini
ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato
ya Serikali ili lengo walilopewa la kukusanya shilingi trilioni 17 liweze kufikiwa.
Mkuu wa Wilaya ya
Shinyanga, Josephine Matiro, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa
Shinyanga, alisema kuwa Serikali mkoani humo itahakikisha kuwa TRA inatimiza
malengo yake ya kukusanya kodi na kumhakikishia Naibu Waziri wa Fedha na Mipango
Dk. Ashatu Kijaji kwamba watasimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ya
Serikali.
CHAMA cha Mapinduzi
(CCM) Zanzibar kimetoa mkono wa pole kwa familia iliyopata ajali ya kuungua
moto nyumba na kusababisha vifo vya watu wanne huko katika kijiji cha Fumba
Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
Akizungumza Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Mabodi wakati wa kuifariji familia hiyo
amesema CCM Zanzibar imesikitishwa sana na tukio hilo kwani limegharimu maisha
ya wananchi wasiokuwa na hatia.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla
Juma Mabodi akiwafariji ndugu na jamaa wa marehemu wa familia iliyopata msiba
huo katika kijiji cha Fumba Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
Dk. Mabodi alisema kwa niaba ya Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein anatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki
wa familia hiyo na kuwasihi waendelee kuwa na moyo wa subra katika
kipindi hichi kigumu cha msiba huo.
“ Kupoteza watu Wanne katika familia
moja ni jambo zito linalotia huzuni lakini tuendelee kuwa wavumilivu
kwani Allah amewapenda zaidi na sisi tuliobaki tuendelee kuwaombea dua
ili wapate makaazi mema na kusamehewa madhambi yao”, alitoa nasaha hizo kwa
maskitiko makubwa Dk. Mabodi.”
Mapema Sheha wa Shehia ya Fumba, Mohamed
Suleiman alifafanua kuwa nyumba hiyo ilianza kuwaka moto majira ya saa 6:15
usiku Oktoba 21 mwaka huu, ambapo wananchi mbali mbali walianza juhudi za
kuzima moto huo na kushindwa kuokoa watu waliokuwa ndani kwani uliku ni mkubwa.
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla
Juma Mabodi Akisalimiana na baadhi ya wananchi na viongozi mbali mbali
walioudhuria katika msiba huo.
Suleiman alisema wakati juhudi za kuzima moto
huo zikiendelea waliwasiliana na Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar ambacho
kilifika na kusaidiana na wananchi hao ambapo walizima moto huo na kukuta watu
wanne tayari wamefariki dunia.
Akithibitisha tukio tukio hiloalisema chanzo
cha moto huo ni hitilafu za umeme zilizoanzia katika waya wa jokofu (Friji)
lililokuwa likifanya kazi wakati wa usiku.
Kamanda Nassir aliwataja watu waliofariki
katika tukio hilo kuwa ni Bahati Ali Ameir (40), Sinawema Abdalla Ali, Hashim
Abdalla Ali (6) na Latifa Mohamed Ali (8).
Alitoa wito kwa wananchi kujenga utamaduni wa
kuzima vifaa vya umeme wakati wa usiku ambavyo havina umuhimu wa kutumiwa
wakati huo ili kuepuka majanga yanayoweza kuhatarisha maisha ya watu.
WAZIRI wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amezungumzia umuhimu
kwa wafanyakazi wote waliopata fursa ya kujenga reli ya kisasa (SGR) kufanya
kazi kwa moyo na uzalendo mkubwa ili kuandika historia katika maendeleo ya
Tanzania.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa kampuni ya Yapi Merkezi Abdullah Kilic, anayejenge reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam-Morogoro yenye urefu wa KM 205 eneo la Soga, mkoani Pwani.
Mbarawa amesema
hayo alipokuwa anakagua ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), inayojengwa usiku na
mchana kuanzia Dar es Salaam-Morogoro
yenye urefu wa KM 205 ambayo kwa kiasi kikubwa ameonesha kurizishwa na kasi
ya ujenzi huo.
“Hii ni fursa
kubwa ambayo mmeipata kujenga mradi mkubwa utakaocha historia katika nchi hii
hivyo fanyeni kazi kwa bidii, weledi na uzalendo”, alisema.
Amewataka viongozi
wa Shirika Hodhi la Rasilimali za Reli (RAHCO), kuwa katika eneo la mradi wakati
wote ili kuhakikisha mkandarasi anapata ushirikiano wa kutosha na hivyo
kuwezesha mradi kukamilika kama ilivopangwa.
Meneja
Mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) Mhandisi Maizo Mgedzi, akifafanua jambo
kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, alipokagua ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es
Salaam-Morogoro yenye urefu wa KM 205 eneo la Soga, mkoani Pwani, inayojengwa
usiku na mchana.
Pia amemuagiza
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa RAHCO Mhandisi Edward Malima, kuhakikisha wanafunzi wa
uhandisi wanapata nafasi ya kutosha ya kushiriki kwa vitendo katika ujenzi huo
ili kuiwezesha nchi kuwa na wataalamu wa kutosha wenye uzoefu kwenye ujenzi na
usimamizi wa miradi ya reli.
“Ongezeni
wahandisi wanafunzi katika mradi huu, nia yetu ni kupata reli lakini pia na
wataalamu wengi katika ujenzi na uendeshaji wa reli”, alisisitiza.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akimpongeza mwanamke anayeendesha mtambo wa kutengeneza tuta la reli ya kisasa (SGR), Miriam Juma alipomkuta saa 4 za usiku akichapa kazi katika eneo la Soga, mkoani Pwani.
Kwa upande wake Malima,
amempongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa kufanya ziara ya
kustukiza usiku ambayo imechochea hamasa kwa wafanyakazi na mkandarasi na
kuahidi kumsimamia mkandarasi kikamilifu
ili mradi huo ukamilike kwa wakati na uwiane na thamani ya fedha.
Muonekano wa Mitambo ya
kisasa inayojenga Reli ya Kisasa (SGR), kutoka Dar es Salaam-Morogoro yenye
urefu wa KM 205 eneo la Soga mkoani Pwani, inayojengwa kwa saa 24.
Takribani
shilingi trilioni 2.8 zinatarajiwa kutumika kkstika ujenzi wa reli hiyo awamu
ya kwaza kati ya Dar es Salaam na Morogoro yenye urefu wa KM 205 itakayowezesha
treni ya umeme yenye kasi ya KM 160 kwa saa kupita na hivyo kuhuisha mfumo wa
usafiri wa reli hapa nchini.
MKUTANO wa Saba wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR)
umefanyika leo tarehe 19 Oktoba, 2017 mjini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo.
Kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Mkutano huo
umetanguliwa na ule wa awali ngazi ya Wataalamu wa Masuala ya Fedha, Wakuu wa
Vyombo vya Usalama, Majeshi na Waratibu wa Nchi (ICGLR National Coordinators)
pamoja na Mawaziri wa Mambo ya Nje.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk.
Augustine Mahiga, ametoa ujumbe akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk. John Pombe Joseph Magufuli mkutanoni hapo.
Mkutano huu umehudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali na Wawakilishi
wao kutoka nchi za Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo, Kenya, Rwanda, Sudani, Sudani Kusini,
Tanzania, Uganda na Zambia ukiwa na ajenda kuu ya kupitia na kujadili hali ya
Siasa, Ulinzi na usalama katika eneo la Nchi za Maziwa Makuu hasa katika nchi
za Burundi, Kongo, Jamhuri ya Kongo, Afrika ya Kati na Sudani Kusini.
Ajenda zingine zilikuwa ni pamoja na kupokea taarifa ya Michango ya
nchi wanachama ambapo Kuhusu
hali ya usalama katika Nchi hizo kwa ujumla iliripotiwa kuwa inaendelea
kuimarika kwa kiwango kikubwa isipokuwa nchini DRC ambapo kwa sasa operesheni zinaendelea
kufanywa na Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC- MONUSCO (FIB) dhidi ya
vikundi vya waasi ndani na nje ya DRC.
Mkutano huu ulifuatiwa na Mkutano wa Nane Wakuu wa Nchi na Serikali wa
Mpango wa Amani na Usalama katika Maziwa Makuu (8th Regional Oversight
Mechanism for the Peace, Security and Cooperation Framework of the DRC and the
Region).
Taasisi zingine za kimataifa zilizoalikwa kwenye Mikutano hii ni pamoja
na Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), na Jumuiya ya Maendeleo Kusini
mwa Afrika (SADC) ambapo ujumbe wake uliongozwa na Katibu Mtendaji wa SADC, Dk.
Stergomena Tax.
AFISA Elimu wa Mkoa wa Dar es salaam Hamis Lissu
ameahidi kutatua kero zote zinazowakabili baadhi ya wamiliki wa Shule
Binafsiinafsi wa mkoa ikiwemo ya tozo kubwa za biashara zinazotozwa shule
hizo .
Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam akizungumza na washiriki wa mkutano uliowakutanisha wamiliki wa shule binafsi mkoa wa Dar es Salaam |
Pia amewaomba wamiliki wa shule hizo kipindi cha likizo wajitolee
kuwafundisha masomo ya sayansi wanafunzi wanaotoka shule za serikali kwa kuwa
wana walimu wengi wa masomo hayo.
Ameyasema hayo leo alipokuwa akifungua Mkutano Maalumu
uliowakutanisha wadau mbalimbali na wamiliki wa shule zilizopo jijini hapa.
Amesema wamiliki wa shule hizo pamoja na shule zao wanapaswa watambaue
huduma wanazopewa ni stahiki hivyo ni sawa wanazopatiwa shule za
Serikali.
“Natamani kuziona shule zote binafsi zikiwa zinazoongoza kutokuwa na
changamaoto zozote kwani tunatambua mchango wa uwekezaji hapa nchini,” amesema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wamiliki wa Shule
Binafsi nchini (TAMONGSCO), Charles Totela ameishukuru Serikali ya mkoa huo
kwani imekuwa ikiwapa ushirikiano wa kutosha.
Mwenyekiti huyo ameiomba Serikali ya mkoa huo kuwaundia dawati la
pamoja litakalowakutanisha viongozi wote wa shule binafsi, za serikali na
watendaji wao ili waweze kukaa pamoja na kujadiliana baadhi ya changamoto ambazo
zimekuwa hazifanyiwi kazi.
Naye Mkurugenzi wa Shule za Al-Muntazir, Mahmood Ladack
amewashukuru wamiliki wa shule hizo kwa kuhitisha mkuatano huo ambao anataraji
utakuwa na manufaa makubwa kwao na taasisi wanazosimamia katika kupambana na
changamoto mbalimbali zinazowakabili.
UONGOZI wa mkoani
Simiyu umembadilishia majukumu ya kazi Tabibu, Laurent Biyengo na
kuwa mlinzi katika lango kuu la kuingilia hospitali kutokana na kushindwa
kuyamudu majukumu ya kitabibu.
Biyengo ambaye anadaiwa kushindwa kuingia kazini
na kwenda kulewa saa za kazi alipokuwa zamu septemba 27 mwaka huu na
kusababisha ujauzito aliokuwa nao Salome John kutoka kwa kushindwa kupatiwa
huduma.
Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika kutoka ndani
ya hospitali hiyo na kuthibitishwa na baadhi ya matumishi wenzake zinaeleza
kuwa tangu aanze majukumu yake hayo mapya sasa ni kipindi cha majuma mawili
akilinda getini.
Wakizungumza na hivi karibuni, baadhi ya
madaktari hao walisema kuwa adhabu aliyopewa ni ya haki kutokana na kitendo
alichokifanya ambacho kinakiuka maadili ya taaluma yao ya utabibu.
“Huyu mwenzetu amepata adhabu ya haki na hii
wamemsaidia sana maana alipaswa kufukuzwa kazi haiwezekani umepangwa kutoa
huduma za kitabibu katika hospitali kubwa kama hii halafu unakwenda kulewa na
kusababisha wagonjwa kutopata huduma, nikukiuka maadili ya kitabibu,”alisema
Daktari mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Walisema kuwa kitendo alichokifanya
kimewapotezea imani kwa wagonjwa wanaofika kupata matibabu katika hospitali
hiyo, huku wengine wakitumia lugha za kuwakejeli na kuwadhihaki jambo ambalo
linawashusha molali ya kazi.
Kwa mujibu wa habari za kuaminika kutoka chanzo
ambacho kilifika katika hospitali ya wilaya ya Maswa na kumshuhudia daktari
huyo akiwa katika lango kuu la kuingilia hospitalini hapo, na
kumwona akufungulia magari na pikipiki zinazoingia na kutoka
sambamba na watu wanaokuja kupata matibabu hata hivyo jitihada za kuongea naye
hazikuzaa matunda baada ya kugoma kuongea.
Akizungumzia suala hilo Mkuu wa wilaya ya Maswa
Dk. Seif Shekalaghe alikiri kwa daktari huyo kubadilishiwa majukumu ya kazi na
kusisitiza kuwa hiyo ni hatua ya awali walizozichukua kutokana na kitendo
alichokifanya.
“Nimeambiwa ya kuwa amebadilishiwa majukumu ya
kazi kutoka kutoa huduma za kitabibu na kuwa mlinzi lakini nahisi kuna hatua
zaidi ya hiyo inatakiwa kufanywa nipeni muda tutapata majibu sahihi,”alisema
Shekalaghe.
Kufuatia tukio hilo,Waziri wa Afya ,Ustawi wa
jamii,Wazee,Jinsia na Watoto,Ummy Mwalimu alimwelekeza Naibu Katibu Mkuu
TAMISEMI Dk. Zainab Chaula kumchukulia hatua.
MAKAMISHINA wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
wametembelea eneo la Njedengwa Mjini Dodoma yanapojengwa majengo ya makao makuu
ya NEC na kuelezea kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo.
Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) Jaji (R), Simistocles Kaijage, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan
Kailima na Mhandisi kutoka Wakala wa Majengo (TBA), Yohana Mashausi
wakiwaongoza makamishna wa NEC kutembelea eneo la mradi wa ujenzi wa majengo ya
ofisi za NEC jana. Mradi huo unafanyika katika eneo la Njedengwa Mjini Dodoma.
(Picha na Abdulwakil Saiboko)
Akizingumza mara baada ya ziara hiyo
iliyoongozwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji (R) Semistocles Kaijage, Mkurugenzi wa
Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima alisema kwamba maendeleo ya ujenzi
yanaridhisha na ujenzi utakamilika kwa muda uliopangwa.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R),
Simistocles Kaijage (wa pili kulia) akifurahia jambo na Mhandisi kutoka Wakala
wa Majengo (TBA), Bw. Yohana Mashausi (kulia) baada ya kupewa maelezo ya mradi
wa ujenzi wa majengo ya ofisi za NEC jana wakati makamishana wa NEC
walipotemdelea mradi huo. Mradi huo unafanyika katika eneo la Njedengwa Mjini
Dodoma na unatarajiwa kukamilika mwakani. (Picha na Abdulwakil Saiboko)
Kailima amesema kwamba awamu ya kwanza ya
ujenzi wa mradi huo ambao unajumuisha majengo matatu utakamilika mwezi Julai,
mwakani.
“Mradi huu una awamu mbili za ujenzi lakini
utatoa majengo makubwa matatu, jengo la kwanza ni jengo kubwa la ofisi litakua
na ghorofa nane, la pili ni jengo la ukumbi wa kutangazia matokea ambao utakua
na uwezo wa kuchukua watu 800, uchaguzi mkuu ujao wa 2020 tunatarajia kutangaza
matokeo kwenye ukumbi huu na pia kuna jengo la maghala ya kuhifadhia vifaa vya
uchaguzi,” amesema Kailima.
Aliongeza kusema “Mradi huu unakwenda vizuri
kwa sababu gharama yake ni takribani shilingi bilioni 13, awamu ya kwanza
itagharimu bilioni 11/- ambayo itahusisha ujenzi wa jengo la ofisi, pia
itajumuisha ujenzi wa sehemu ya jengo la kituo cha kutangazia matokeo na
maghala.
Awamu ya pili ambayo itagharimu bilioni 2/-
itakua imekamilika mwaka 2018. Kuanzia mwenzi Agosti 2018 Tume tutaanza kuhamia
Dodoma,” amesema.
Kutoka kushoto ni Mhandisi kutoka Wakala wa Majengo (TBA), Yohana
Mashausi akitoa maelezo ya mradi wa ujenzi wa ofisi za Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) kwa makamishna wa tume
hiyo walioongozwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R),
Simistocles Kaijage, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima na Makamu
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid. Ujenzi huo unaoendelea
katika eneo la Njedengwa Mjini Dodoma unatarajiwa kukamilika mwakani. (Picha na
Abdulwakil Saiboko).
Akizungumzia suala la bajeti ya ujenzi wa
majengo hayo, Kailima amesema fedha zipo na zitakua zikitolewa kadri
zitakavyohitajika.
Mwanzoni akiwatembeza makamishna wa tume
kwenye eneo la mradi, Mkandarasi Msimamizi kutoka Wakala wa Majengo (TBA),
Mhandisi Yohana Mashausi amesema ujenzi huo umechukua muda mrefu kwenye eneo la
msingi kwa kuwa eneo hilo lina ardhi yenye mwamba mgumu sana.
Mhandisi Mashausi amesema kwamba TBA pia
imechukua tahadhari kubwa katika ujenzi wa msingi imara kwa kuzingatia hali ya
kijogirafia ya Dodoma ambako kuna hatari ya kukumbwa na matetemeko ya ardhi.
SERIKALI imesema ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA), unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu ambapo kwa
sasa umefika zaidi ya asilimia Tisini.
Meneja Miradi wa Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Mhandisi Mathew Ndossi, akimuonesha
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius
Kwandikwa (Mb), (Kushoto), upanuzi wa maegesho ya ndege uliofanyika uwanjani
hapo.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Elius
Kwandikwa, mara baada ya kukagua ukarabati wa jengo la kupumzikia abiria na
upanuzi wa maegesho ya ndege katika uwanja huo leo mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elius Kwandikwa (Mb),
akikagua maboresho ya mfumo wa majitaka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA), alipofika uwanjani hapo kujionea hatua zilizofikiwa za
ukarabati wa uwanja huo.
"Nimeridhishwa na ukarabati unaoendelea katika uwanja huu na nafikiri
mmejionea wenyewe kazi inaendelea vizuri, hivyo naamini kutokana na hali hii
kazi itakamilika hivi karibuni, amesema Naibu Waziri Kwandikwa.
Naibu Waziri huyo amefafanua kuwa ukarabati huo ambao pia umehusisha
maboresho ya mfumo wa maji taka unalenga kuleta tija kwa mkoa huo na Taifa kwa
ujumla kutokana na kuwepo ongezeko la abiria, huduma za kijamii na kibiashara.
Mafundi wakiendelea na
ukarabati katika jengo la abiria la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA). Ukarabati huo umefika zaidi ya asilimia Tisini na unatarajiwa kukamilika
mwezi Desemba mwaka huu.
Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kukarabati na kujenga viwanja vya
ndege nchini ili kurahisisha huduma za usafiri wa anga kwa wananchi wake lengo
likiwa ni kuchochea fursa za kiuchumi ambazo zitasaidia kulipeleka Taifa katika
uchumi wa kati.
Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius Kwandikwa,
akifafanua jambo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoani Arusha,
Mhandisi Johny Kalupale, alipokagua barabara ya Sakina – Tengeru (KM 14.1) na
Barabara ya Mchepuko ya Arusha (Arusha Bypass KM 42.4) mkoani Arusha.
Kwa upande wake, Meneja Miradi wa KIA, Mhandisi Mathew Ndossi,
amesema kuwa maegesho yatakapokamilika yatakuwa na uwezo wa kuegesha jumla ya
ndege kubwa 11 kwa wakati mmoja badala ya 6 zinazoegeshwa sasa.
Ameongeza kuwa abiria wanatarajiwa kuongezeka kutoka laki nane kwa mwaka
hadi kufikia milioni moja na laki mbili mara baada ya kukamilika kwa uwanja
huo.
Muonekano wa Barabara ya
Sakina – Tengeru (KM 14.1), mkoani Arusha, ambayo imekamilika kwa kiwango cha
lami. Kukamilika kwake kumesaidia kupunguza ajali na msongamano katika eneo
hilo.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kwandikwa amekagua barabara ya Sakina
- Tengeru (km 14.1) na barabara ya mchepuko ya Arusha (Arusha Bypass km 42.4)
ambapo amesema kuwa kukamilika kwa barabara ya Sakina - Tengeru ni
mkombozi mkubwa kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na wageni wanaoingia katika mkoa
huo kwani kumepelekea kupungua kwa ajali na msongamano wa
magari katika eneo hilo.
Ametoa wito kwa wananchi kuzitunza barabara na kutunza mazingira
yanayozunguka barabara hizo ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwa vizazi vya
sasa na vijavyo.
Muonekano wa Daraja la
Ndurumo lililopo katika barabara ya Sakina
– Tengeru (KM 14.1), mkoani Arusha.
Awamu ya pili ya mradi huo sehemu ya barabara ya mchepuo ya Arusha (Arusha Bypass), inayofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), inatarajiwa kukamilika mwakani na kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 67.Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Arusha Mhandisi, Johny Kalupale, amemhakikishia Naibu Waziri huyo kufanya kazi kwa ubora na kwa weledi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kuwajengea wananchi miundombinu bora na ya kisasa.
Naibu Waziri Kwandikwa amemaliza ziara ya kikazi katika mkoa wa
Kilimanjaro na Arusha ambapo amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na
Wizara yake.