Habari Mpya

Tuesday, 5 September 2017

Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) inatekeleza miradi miwili ya taa za kuongozea magari na abiria (traffic lights) jijini Tanga katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani

Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakifunga mabomba ya chuma kwa ajili ya kusimika mfumo wa taa za kuongozea magari katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo na utatumia umeme jua
Akiongea na Waandishi wa Habari Meneja wa Kikosi cha Umeme TEMESA Mhandisi Pongeza Semakuwa alisema miradi hii miwili ya taa za barabarani hapo Tanga inahusisha taa za kuongozea magari pamoja na zile za kuongoza waenda kwa miguu kuvuka makutano hayo ya barabara. Taa hizo zitakuwa zikitumia umeme jua, nishati ambayo itaziwezesha kufanya kazi muda wote hata pale umeme wa TANESCO unapokuwa na hitilafu.
          Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakiunganisha nyaya kwenye “Panel za Solar” zitakazotumika katika mfumo wa taa za kuongozea magari na abiria (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani Jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati umeme jua.
Nae Mbunge wa Jimbo la Tanga mjini Alhaj Mussa Mbaruku  ambae alipita katika eneo la mradi la makutano ya Barabara ya Pangani na Taifa maarufu kama “Taifa/Ring Junction” kujionea utekelezaji huo wa mradi wa Serikali, alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutapunguza ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikitokea kwenye makutano ya barabara hizo na vile vile kuufanya mji wa Tanga kuwa wa kisasa zaidi.
Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakifunga taa za kuongozea magari (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati ya umeme jua.
Kwa upande wake Meneja wa TEMESA Tanga Mhandisi Margareth Gina alisema kuwa miradi hiyo ya usimikaji wa taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu jijini Tanga imeiingizia TEMESA jumla ya shilingi za kitanzania milioni 434 fedha za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitakazolipwa kwa TEMESA kupitia ofisi ya Mkurugenzi wa jiji la Tanga. Aliongeza kuwa miradi yote miwili iko mbioni kukamilika mapema mwezi huu.
Mbunge wa Tanga Mjini Alhaj Mussa Mbaruku akiongea na watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) alipofika katika eneo la mradi wa kusimika taa za barabarani katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na pangazi pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati ya umeme jua. kutoka kushoto ni Mhandisi Zuhura Semboja, Mhandisi Pongeza Semakuwa pamoja na Mhandisi Margaret Gina.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © 2025 Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -