Habari Mpya

Friday, 17 November 2017

WATU 40 wa Kitongoji cha Isumbi katika Kijiji cha Igung’hwa Kata ya Kinaga katika Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga, wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo baada ya kudaiwa kula kiporo na mboga za majani aina ya mgagani.

Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kinaga, Paul Damasi alisema wananchi waliolazwa katika Hospitali ya Mji wa Kahama ni wale waliokula kiporo cha ugali na mboga za majani aina ya mgagani waliouita “mchicha.”

Aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na wananchi katika msiba uliotokea nyumbani kwa Salum Manyanda na kuongeza kuwa asilimia kubwa ya watu waliougua ghafla baada ya kula chakula hicho ni wanawake.

Ofisa Mtendaji wa Kata huyo alisema tukio hilo lilitokea juzi saa tano asubuhi baada ya waombolezaji kula chakula kilichobakia jana ya siku hiyo huku akieleza kuwa wote waliougua ghafla walikimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kahama kupatiwa matibabu.


“Idadi ya watu haijafahamika ila nimepewa taarifa kuwa ni zaidi ya wakinamama arobaini ndiyo waliokimbizwa katika Hospitali ya Mji wa Kahama, msiba ulitokea Novemba 14, kama unavyojua vijijini bado kuna ile tabia ya msiba unapotokea akinamama wanapika chakula nyumbani kisha wanapeleka msibani.

Leave a Reply

Subscribe to Posts | Subscribe to Comments

- Copyright © Mito Ya Baraka Morogoro - Mito Ya Baraka Morogoro - Powered by Blogger - Designed by Peter Mwamkamba -