Habari Zote
Archive for August 2017
Serikali imesema kuwa imetumia
shilingi Bilioni 85 kupeleka mawasiliano vijijini kupitia Mfuko wa Mawasiliano
kwa Wote (UCSAF) kwa kuzipatia ruzuku kampuni za simu za mkononi ili
kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma za mawasiliano.
Hayo yameelezwa na
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani wakati
akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)
kwenye Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu mjini Dodoma.
“Mfuko huu unaendelea
kuhakikisha kuwa mawasiliano bora yanafika katika maeneo mengi nchini hususan
vijijini na kwenye maeneo ambayo hayana mvuto wa kibiashara ambapo Takwimu
zinabainisha kuwa, tayari mawasiliano
yamefikishwa kwenye kata 443, vijiji 1,939 kuanzia mwezi Machi 2013 hadi Julai mwaka huu”,
amefafanua Naibu Waziri Ngonyani.
Ameongeza kuwa tayari
Mfuko umetiliana saini mkataba na kampuni za simu za mkononi mwezi Agosti mwaka
huu kuhakikisha kuwa zinapeleka mawasiliano kwenye kata nyingine 75 na vijiji
154.
Pia, ametanabaisha kuwa
hadi hivi sasa asilimia 94 ya wananchi wanapata huduma ya mawasiliano nchini na
kuongeza kuwa, Serikali kupitia mkataba wake na Kampuni ya Simu ya Halotel
imefikisha mawasiliano kwenye jumla ya vijiji 3,069 kati ya vijiji 4,000 tangu
walipoanza utekelezaji wa jukumu hilo mwezi Novemba, 2015 na wanatarajia
kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.
Kwa upande wake, Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu Mhe. Moshi Kakoso,
amezitaka kampuni za simu za mkononi zinazopeleka mawasiliano vijijini na
maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara ambazo zinapatiwa ruzuku na Serikali kuhakikisha
kuwa zinatoa taarifa sahihi kwa Mfuko huo ikiwemo hatua zilizofikiwa za ujenzi na
usimikaji wa minara na uwepo wa mawasiliano kwenye vijiji husika.
Amewataka UCSAF kujitangaza na kuweka mabango
yao kwenye minara yote nchini iliyojengwa kupitia ruzuku ya Serikali ili kuwawezesha
wananchi kutambua uwajibikaji wa Serikali katika kufikisha mawasiliano kwa
wananchi wake.
Naye, Naibu Katibu Mkuu
wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Eng.
Angelina Madete, amesema kuwa Wizara kupitia UCSAF itahakikisha kuwa kila
mwananchi anafikiwa na mawasiliano kuendana na jukumu la msingi la Mfuko huo la
kufikisha mawasiliano kwa wote.
Mtendaji Mkuu wa Mfuko
huo Eng. Peter Ulanga, amewahakakikishia wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu
ya Miundombinu kuwa Taasisi yake itashirikiana na wataalam kutoka Ofisi ya
Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mamlaka ya Mawasiliano
Tanzania (TCRA), kuhakiki kazi zilizofanywa na kampuni za simu za mkononi za
ujenzi na usimikaji wa minara na uwepo wa mawasiliano kwenye vijiji mbalimbali
nchini.
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Mahakama ya Tanzania
inakusudia kuanzisha kituo cha Mafunzo kwa ajili ya watumishi wake pamoja na
wadau ili kuwaongezea ujuzi utakaosaidia kuboresha huduma zinazotolewa na Mahakama.
Kituo hicho
kinachojengwa katika eneo la Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam
kitawaunganisha watumishi wa Mahakama na wadau katika mafunzo kwa njia ya video
(video conferencing).
Akizungumzia Kituo
hicho, Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof Ibrahim Hamis Juma alisema ujenzi
wa kituo hicho ni sehemu ya Maboresho ya huduma za Mahakama ambacho pia wadau wa
Mahakama watakuwa ni sehemu ya mafunzo yatakayokuwa yakitolewa.
Alisema badala ya
Majaji, Mahakimu, watumishi na wadau wa Mahakama kwenda kupata baadhi ya mafunzo
kwenye chuo cha Uongozi wa Mahakama- Lushoto (IJA), baadhi ya mafunzo watakuwa
wakiyapata katika kituo hicho.
Naye Mratibu wa Mpango
Mkakati wa Mahakama pamoja na maboresho ya Huduma za Mahakama Mhe. Zahara
Maruma alisema ujenzi wa kituo hicho ni utekelezaji wa nguzo ya tatu ya mpango
Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania ambapo kupitia nguzo ya pili ya
Mpango huo, Majaji na Mahakimu hupatiwa mafunzo mbalimbali ili kurahisisha
upatikanaji wa haki kwa wakati.
Akizungumzia nguzo ya
tatu ya Mpango huo, Mhe. Maruma alisema nguzo hiyo inahusiana na urejeshaji wa
imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za
Mahakama ambapo kupitia kituo hicho wadau wa Mahakama watahusishwa kwenye
Mafunzo mbalimbali ili kurahisisha suala la upatikanaji wa Haki.
Kuhusu suala la
matumizi ya Teknolojia ndani ya Mahakama, Mratibu huyo alisema hivi sasa
Mahakama inao mpango wa kujenga vituo vya aina hiyo kwenye maeneo mbalimbali
nchini kwa lengo la kuunganisha Mahakama zote nchini kwa njia ya video (video
conferencing).
Ujenzi wa kituo cha
Mafunzo cha Mahakama ulioanza hivi karibuni kwa ushirikiano kati ya Mahakama ya
Tanzania na Benki ya Dunia unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi za
kitanzania milioni 78. Aidha, Jengo la kituo hicho cha mafunzo linajengwa kwa
kutumia teknolojia ya gharama nafuu iitwayo Moladi na linatarajiwa kukamilika
ndani ya wiki nane.
WAZIRI mkuu Kassim
Majaliwa amewataka Watanzania wote wahakikishe wanaboresha mshikamano wao
pamoja na kuimarisha uzalendo kwa Taifa lao.
![]() |
Mji wa Cuba |
Ametoa kauli hiyo jana
jioni (Jumapili, Agosti 20, 2017) wakati akizungumza na wanafunzi wa Kitanzania
wanaosomea udaktari nchini Cuba.
Majaliwa ambaye yuko
nchini Cuba kwa ajili ya
ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Alisema uzalendo kwa Taifa ni jambo muhimu kwa sababu ya kukosa fursa nyingi za
kimaendeleo kutokana na baadhi ya wananchi kutokuwa wazalendo kwa Taifa lao.
Kutokana na hali hiyo
Serikali inawasisitiza Wananchi kuwa wazalendo na washirikiane kuhakikisha
fursa za kimaendeleo zilizoko nchini zinaendelezwa.
Alisema Serikali
inatekeleza miradi mingi kwa lengo la kukuza uchumi kutoka chini kwenda wa
katikupitia ushirikiano.
Pia Waziri Mkuu
alitumia fursa hiyo kuwasihi wanafunzi hao kuzingatia sheria za nchini waliyoko
pamoja na kukumbuka kurudi nyumbani mara wamalizapo masomo yao.
Alisema Serikali
inatambua uwepo wao wa kimasomo nchini Cuba na kwamba inatarajia kupata mchango
mkubwa kutoka kwao punde wamalizapo masomo yao.
“Nawaomba msome
kwa bidii na mfaulu mitihani yenu. Elimu yenu iwasaidie katika ajira na muweze
kurejesha mikopo mliyopewa na Serikali ili iwanufaishe wengine.”
Katika hatua nyingine,
Waziri Mkuu aliwataka Mabalozi wote wanaoiwakilisha Tanzania katika mataifa
mbalimbali kuhakikisha wanatangaza vivutio vya utalii.
Alisema Tanzania
imejaaliwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, hivyo ni vema Mabalozi
wakavitangaza jambo ambalo litasaidia kuongeza idadi ya watalii wanaokuja
nchini.
Miongoni mwa vivutio
vya utalii vilivyoko nchini ni pamoja na mlima Kilimanjaro, visiwa vya
Zanzibar, mbuga mbalimbali zenye wanyama wa aina tofauti tofauti.
Awali Mwenyekiti wa wanafunzi hao, Goodchance
Tarimo alimuhakikishia Waziri
Mkuu kwamba watarejea nyumbani mara baada ya kumaliza masomo yao nchini humo.
Alisema wao wana imani kubwa na Serikali na
wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na viongozi wa Taifa kwa lengo la
kuboresha maendeleo pamoja na kukuza uchumi.
“Tunapongeza jitihada za Serikali ya Awamu ya
Tano katika kujenga uchumi wa viwanda, mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi
na ujenzi wa miundombinu ya kisasa”
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi ameiomba Benki
ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kukopesha wakulima wa mazao ya ufuta na
mihogo ili waweze kulima kilimo cha kisasa na cha kibiashara hasa kwa wakulima
wadogo wadogo wa mkoani humo.
Zambi alitoa wito huo wakati wa mkutano wa Wadau wa
Korosho na Ufuta Mkoa wa Lindi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Zambi alisema kuwa mkoa wa Lindi ni mkoa
uliojaaliwa katika kuzalisha mazao ya ufuta na mihogo lakini changamoto kubwa
ni mtaji wa kulima kibiashara ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya
nchi.
“Wakulima wa mkoa wa Lindi wapo tayari kushiriki
katika kuleta mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha
kibiashara lakini kwa sasa suala la mtaji wa kilimo cha kibiashara ni
changamoto kubwa,” alisema Zambi.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Lindi alisema kuwa ili
kuwezesha wakulima hao kulima kibiashara Benki ya Kilimo ina wajibu wa kutoa
mikopo yenye riba nafuu ili kuhamasisha wakulima hao wa mkoa wa Lindi waweze
kuongeza uzalishaji wenye tija katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini
mkoani humo.
Aliongeza kuwa kama TADB itaboresha upatikanaji wa
mikopo na huduma za kifedha kwenye miradi ya maendeleo ya Kilimo kwa riba nafuu
zilizo chini ya viwango vya kibiashara kwenye soko kutawezesha wakulima wa
Tanzania kufikia uchumi wa kati kama ilivyolengwa na Serikali ifikapo mwaka
2015.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Francis
Assenga alisema kuwa Benki ya kilimo ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima
wadogo wadogo waliokuwa kwenye vikundi ili waweze kukopeshwa.
Assenga aliongeza kuwa Benki ya Kilimo pia ipo
tayari kuwekeza kwenye miradi ya maendeleo ya Kilimo kwa kuipatia mikopo yenye
riba nafuu zilizo chini ya viwango vya kibiashara kwenye soko.
“Kwa kutambua umuhimu wa wakulima wadogo wadogo
nchini TADB imedhamiria na kujizatiti kuhakikisha inachangia kwa kiasi kikubwa
katika kuleta Mapinduzi yenye tija
katika Sekta ya Kilimo nchini kwa kusaidia upatikanaji na utoaji wa fedha ikiwa
ni pamoja sera nzuri zitakazosaidia maendeleo ya kilimo nchini,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema kuwa Benki yake
inaandaa mfumo mahususi wa uratibu kwa kushirikiana na halmashauri za mikoa ili
kuhakikisha kuna upatikanaji wa fedha kwa ajili ya minyororo ya ongezeko la
thamani kwa mazao ya Kilimo nchini.
“Tupo tayari kusaidia uzalishaji kwenye hatua mbali
mbali za uongezaji wa thamani, hadi masoko ya bidhaa za mwisho hadi kumfikia mlaji na kusaidia kuwaunganisha
wakulima na masoko kupitia halmashauri zao,” alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa
TADB, Augustino Chacha alisema kuwa TADB inalenga kuongeza upatikanaji wa
huduma zisizo za kifedha kwa wakulima kama vile kujengewa uwezo juu ya uandaaji
wa andiko la miradi ya Kilimo, pamoja na upatikanaji wa taarifa za masoko,
usimamizi wa biashara, mafunzo juu ya miradi ya Kilimo na mbinu za majadiliano
ya mikataba.
“Tupo tayari
kutoa mikopo kwa ajili ya kuwanyanyua wakulima kama ilivyolengwa na Serikali
kupitia mikopo ya pembejeo kuongeza tija kwenye uzalishaji, miundo mbinu ya
umwagiliaji na ununuzi wa zana za kilimo,” alisema.
Chacha aliongeza kuwa kwa upande wa mikoa ya kusini
Benki ya Kilimo imejipanga kueendeleza miundombinu ya umwagiliaji na maghala
pamoja na uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya korosho na mihogo na kuimarisha
viwanda vya kubangua mazao ya korosho, na kusindika ufuta, mihogo.
Chacha aliongeza kuwa Benki imejipanga kuwezesha
uanzishaji wa mashamba mapya na ya kisasa ya mihogo, korosho na ufuta mkoani
Lindi.
KUTOKANA na vitendo vya unyanyasaji wa
kijinsia kuendelea kutokea katika jamii yetu, katika maeneo mbalimbali hapa
nchini, mashirika na asasi mbalimbali, zikiwemo za serikali na binafsi zimekuwa
zikiendelea kutoa elimu kwa jamii ili iweze kuachana na vitendo hivyo
unavyovota ni vikinyama
![]() |
Mwanamke mmoja akitoka shambani kulima huku akiwa amebeba mzigo mkubwa wa kuni, mtoto mgongoni na mwingine akiwa amemshikilia mkono. mume wake amemwachia kufanya kazi zote. Huo ni ukatili wa kijinsia |
Mbali na kutoa elimu hiyo pia asasi na
mashirika hayo yamekuwa yakitumia fursa hiyo kuwakumbusha wanajamii madhara ya
ukatili huo, ikiwa ni pamoja na adhabu inayotolewa kwa mtu au kikundi chochote
kilichofanya ukatili wa kijinsi dhidhi ya mtu au watu furani.
Lakini pamoja na kutolewa kwa elimu ndani ya
jamii yetu baadhi ya watu wamekuwa na vichwa vigumu kuachana na vitendo hivyo
na badala yake kila kukicha wamekuwa wakiendesha vitendo hivyo vya ukatili wa
kijinsia dhidi ya wananchi wenzao, wasiostahili adhabu hiyo.
Mara kwa mara vitendo vya ukatili wa kijinsia
vimekuwa vikisikika kutokea kwa wanawake, pamoja na watoto. Lakini pia kwa siku
za hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu tunaambiwa baadhi ya
wanawake nao wameonekana kuwa wanyama kwa kufanyia ukatili wa kijinsia waume
zao.
Baadhi ya wanaume wamekuwa wakiwafanyia
ukatili wa kijinsia wake zao, kwa sababu ya mfumo dume, kwa kuwapa kipigo
kikali, ukatili wa kingono na ukatili wa kila aina kwa kutumia mfumo huo dume.
Aidha, watoto nao wamekuwa wakifanyiwa vitendo
hivyo vya ukatili, vikiwemo vya kupigwa pindi wanapopatikana na makosa ambayo
hata adhabu yake ilitakiwa kuonywa tu, kwa mfano mtoto anapokomba mboga
chunguni ama kwa kusikia njaa ama vinginevyo, ama anapopoteza fedha alizopewa
kwa ajili ya kununua kitu furani dukani, utakuta mzazi au mlezi anampatia
adhabu kali ambayo haiendani kabisa na umri wake.
Wazazi au walezi wengine wamekuwa wakiwapatia
adhabu ya kuwafunga na kamba mikono watoto wao na kisha kuwachoma na
kuwasababishia majeraha mwilini.
Hali hiyo ya ukatili ndiyo inayoweza kumshinda
mtoto husika na kuamua kukimbilia mitaani, na kuzalisha mtoto wa mitaani ambaye
kwa namna nyingine maisha yanavyozidi kuwa magumu kwake hataimaye uamua
kujiingiza kwenye makundi ya kiuharifu na kasha kuiishia jela au kuuawa na
wananchi wanaojichukulia sheria mikononi pindi wanapomtuhumu kutenda kosa
lolote la kiuharifu.
Lakini pia wazazi ama walezi wengine wamekuwa
wakifanya ukatili kwa watoto, ambao ni wakuwanyima haki yao ya msingi ya kuwapatia
elimu, ambayo ingemsaidia katika maisha yake ya baadaye.
Ama wazazi na walezi wengine wamekuwa
wakiwatumikisha watoto wao ambao umri wao hasa unafaa kuwa shule kwa kazi
ambazo haziendani na umri wao, kwani baadhi yao uwatumikisha katika kazi za mashambani,
uwatumikisha katika kazi za uvuvi, uchungaji wa mifugo, kazi za migodini na
kazi nyingine hatarishi kwa maisha yao.
Kwa mfano mimi hainiingii akilini kumtumikisha
mtoto mwenye umri wa miaka saba katika kazi ya uvuvi, kwani ajali ya kuzama mtumbwi
ikitokea, kamwe mtoto huyo hawezi kujiokoa kwa sababu hajui hata kuogelea
kulingana na umri wake kuwa mdogo. Kwa jinsi hiyo hicho ni kitendo cha kumtoa
kama sadaka mtoto mwenye umri huo.
Pia baadhi ya wanaume wanawafanyia vitendo vya
ukatili wa kijinsia wake zao, kwani utakuta mwanaume kazi yake ni kukaa
vijiweni tu muda wote akipiga soga, kuanzia asubuhi hadi jioni. Na kazi ya
shambani au ya uzalishaji mali anamwachia mwanamke na watoto wake pekee.
Baadhi ya wanaume hao wamekuwa ama
wakikalia kulewa pombe tu na muda wa chakula unapowadia urejea nyumbani na
kudai chakula tena kwa sauti kubwa, ilihali hajui chakula hicho kimedhalishwa
kutoka wapi na hata hiyo mboga anayoitumia kulia hajui imenunuliwa na nani?
Lakini bila soni mwaume mtu mzima ujikalisha kwenye meza na kuanza kubugia
chakula hicho kana kwamba kakizalisha yeye.
Na kibaya zaidi anapokuta mwanamke hajaandaa
chakula, ugeuka kuwa mbogo na kuanza kumtolea matusi na kejeri na hata
kumshushia kipigo kikali kama kwamba ni mbwa mwizi.
Wakizungumza kwa nyakati na maeneo tofauti na
mwandishi wa makala hii, baadhi ya wanawake wilayani Bunda, Mara, walisikika
wakisema kuwa hata wakati wa mavuno, licha ya waume zao kutoshiriki kikamilifu
katika shughuli za kilimo hicho, waume zao wamekuwa wakinyang’anywa fedha zote
walizouza mazao yao na kupewa kamgao kidogo tu, nyingi zikichukuliwa na waume
zao na kwenda kufanyia mambo ya starehe ukiwemo unywaji wa pombe na vimwana
vingine vya pembeni maarufu nyumba ndogo.
Mashirika pamoja na asasi mbalimbali za hapa
nchini na hata nje ya nchi zimekuwa zikijitahidi sana kuhakikisha vitendo
hivyo vinakomeshwa ndani ya jamii yetu, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua
za kisheria wale wote wanaoendesha vitendo hivyo.
Nao baadhi ya kina mama wamekuwa wakiwafanyia
unyama usiovumiliwa watoto wao, tena wengine wakisikika wakisema si ni mwanganu
hata kama ni kimuua. Labda hapa niwakumbushe akinamama wa aina hiyo kwamba
mtoto ukisha mzaa ni wa serikali, iwapo ukimfanyia ukatili wa aina yoyote
sheria itachukuliwa dhidi yako bila kujali kwamba wewe ndiye uliyemzaa.
Kutokana na elimu inayotolewa na mashirika,
pamoja na asasi hizo, hivi karibuni serikali wilayani Bunda mkoani Mara,
ililipongeza shirika lisilokuwa la kiserikali la Zinduka lililoko wilayani
humo, linalofadhiliwa na shirika la The Foundation For Civil Society, kwa
kuwapatia wananchi elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ili vitendo
hivyo viweze kukomeshwa ndani ya jamii.
Pongezi hizo zilitolewa na mkuu wa wilaya ya
Bunda, Lydia Bupilipili, aliyewakilishwa na katibu tarafa cha Nansimo, Jonas
Nyaoja, kwenye mafunzo ya kupinga vitendo hivyo.
Mafunzo hayo ambayo yalikuwa ni mwendelezo wa
mafunzo mengine ambayo yamekwishafanyika, yalifanyika katika ukumbi wa kituo
cha walimu katika mji mdogo wa Kibara, uliko katika makao makuu ya jimbo la
Mwiabara.
Mkuu huyo wa wilaya ya Bunda alisema kuwa
serikali wilayani hapa inatambua mchango mkubwa wa shirika hilo katika kutoa
elimu juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, ili jamii iweze kupata uelewa na
kuachana na vitendo hivyo.
“Serikali
wilayani Bunda inatambua mchango mkubwa unaaotolewa na shirika hili la Zinduka
katika kutoa elimu kwa jamii juu ya ukiukwaji haki na unyanyasaji wa kijinsia.
Sasa elimu hii wananchi wetu wakiipata itawasaidia kubadilika na kuacha vitendo
hivyo” alisema Nyaoja kwa niaba ya DC Bupilipili.
Aidha, baadhi ya wadau mbalimbali wanaopinga
vitendo hivyo wilayani hapa, pia wamelishukuru shirika hilo kwa kuwapatia
mafunzo hayo kwa sababu vitendo vya ukatili wa kijinsi vimekithiri sana ndani
ya jamii yetu, ukiwemo ukatili wa kiuchumi pamoja na ule wa tendo la ndoa.
Wadau hao ambao ni pamoja na wazee wa mila,
wazee maarufu, viongozi wa madhehebu ya dini, vyama vya siasa, watendaji wa
vijiji na kata, pamoja na wenyeviti wa vijiji, walisema kuwa Shirika la Zinduka
limejikita sanan katika kutoa elimu hiyo kwa jamii.
Waliyaomba mashairika mengine kuiga mfano huo,
kwani wananchi wengi wamekuwa wakiendesha vitendo hivyo kwa sababu ya kukosa
uelewa na kwamba ni shirika la kwanza kufika mkatika maeneo yao na kuwapatia
elimu hiyo.
Walisema kuwa ukatili mwingine ni ubakaji wa
wanawake, utumikishaji wa watoto wadogo kwenye shughuli hatarishi ambazo
haziendani na umri wao, ukatili wa kutokupeleka watoto shule hususani wa kike,
pamoja na unyanyasaji wanawake na wanaume ndani na hata nje ya ndoa.
Waliongeza kuwa ukatili mwingine ufanywa na
wanaume kuachia shughuli za kilimo na uzalishaji mali wanawake tu, huku wanaume
wengi wakikalia ulevi na uzululaji, ambapo nyakati za chakula ufika majumbani
mwao na kudai chakula tena kwa kuamrisha, ambapo wanawake wanaposema hakuna
chakula uambulia kichapo au matusi ya uzalilishaji.
Walisema kuwa wamridhika na mafunzo hayo
ambayo yamewapatia mwanga, ambapo wataisambaza elimu hiyo katika maeneo yao ili
jamii iweze kubadilika.
Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika
la Zinduka, mhasibu wa shirika hilo, Godfrey Anatory, alisema kuwa wanatoa
mafunzo hayo kwa makundi mbalimbali ya kijamii katika kata tisa za jimbo la
Mwibara na kwamba katika awamu ya kwanza walitoa mafunzo hayo katika kata 13 za
majimbo ya Bunda na Bunda mjini.
“Mafunzo haya tunayaendesha kwa kata tisa za
jimbo la Mwibara, lakini pia mafunzo kama haya tulikwishayaendesha katika kata
13 za majimbo ya Bunda na Bunda mjini. Na baadaye tuendesha mafunzo haya kwa
viongozi mbalimbali wakiwemo maasikari polisi, mahakimu na wanasheria, ili
jamii iweze kujua athari za ukatili wa kijinsia na adhabu yake” alisema.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dk. Stanely
Maendeka, alisema kuwa malengo ya mafunzo hayo ni kupata uelewa sahihi wa dhana
za kijinsia na dhana ya ukatili wa kijinsia, na kupata uelewa na uwezo wa
kutetea na kukomesha ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.
Dk. Mahendeka aliyataja maelengo mengine kuwa
ni pamoja kurekebisha mapendekezo ya awali ya mradi, ili ibebe shughuli
zinazogusa kukomesha ukatili wa kijinsia, kurekebisha bajeti iweze kuingiza au
kuchukuwa shughuli zilizopendekezwa, kukomesha ukatili wa kijinsia na kuweza
kutekeleza mradi vizuri zaidi na kupata matokeo yaliyotarajiwa.
Mkurugenzi wa shirika la Zinduka Maximillian
Madoro, aliwaambia waandishi wa habari kuwa wamekuwa wakitoa mafunzo na elimu
mara kwa mara kwa jamii, ili kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsi katika
wilaya ya Bunda, mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla vitokomezwa.
Madoro amesema kuwa kupitia elimu hiyo kwa
kiasi furani jamii imekwisha badilika na kuachana na vitendo hivyo ingawa bado
kuna changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika baadhi ya wanajamii na
kwamba pamoja na changamoto hizo wanaendelea kutoa elimu hiyo ili kufikia
malengo yao ambayo kikubwa ni kutokomeza vitendo hivyo.
Kwa kumalizia makala yangu napenda
kuwakumbusha wananchi wote kwamba tushirikiane na serikali pamoja na mashirika
kama haya ya Zinduka, kupinga vitendo hivi vya ukatili wa kijinsia, kwani pia
vinavunja haki za msingi za binadamu.
Wote kwa pamoja tukipiga kelele na
kukemea vitendo hivi, ikiwa ni pamoja na kuwafichua ama kuwataja bayana wale
wote wanaoendesha vitendo hivi, vikiwemo na vile vya kukata watu wenye ualbino
viungo vyao na kukata mapanga na kuwaua wazee wenye macho mekundu eti kwa imani
ya ushirikina, hakika vita hii tutaishinda. Na kuwa na jamii iliyostarabika.
Pia tutowe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi
na usalama, pindi tunaposhuhudia matukio kama hayo ndani ya jamii yetu, basi
tuwe mstari wa mbele kutoa ushahidi mahakamani ili mhusika au wahusika waweze
kuchukuliwa hatua na kuhukumiwa adhabu anayostahili kulingana kosa lake
alilotenda kwa mjibu wa sheria za nchi yetu.
Benki ya Maendeleo ya
Kilimo Tanzania (TADB) imewaasa wakulima wa korosho nchini kuongeza uzalishaji
wa korosho ili kuchangamkia fursa za masoko ya zao hilo linalohitajika zaidi
katika masoko ya Marekani, Vietnam na India.
Wito huo umetolewa jana
na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga wakati akifungua
Warsha ya Siku ya Wadau wa Vyama vya Ushirika inayoendelea katika Ukumbi wa
Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Assenga alisema kuwa
mahitaji ya korosho ni makubwa sana katika soko la dunia hivyo wakulima wa zao
hilo hawana budi kujizatiti ili kuhakikisha wanazalisha kiasi kikubwa cha
korosho ili kufikia au kuzidi malengo ya mavuno kwa msimu ujao ambayo
yanakadiriwa kufikia kati ya tani laki tatu (3) hadi laki nne (4) ukilinganisha
na takribani tani laki mbili na nusu kwa msimu uliopita.
Assenga alisema kuwa
korosho ni zao la kimkakati ambalo likiwekezwa kwa usahihi linaweza kunyanyua
uchumi na kipato kwa wakulima wa mikoa ya kusini na pwani ambao niyo ni
wazalishaji wakuu wa zao hilo.
“Nawaasa mujitahidi
kulima kisasa ili kuweza kufikia au kuvuka malengo ya mavuno ya msimu huu hali
itakayowaongezea kipato hivyo kufikia malengo ya serikali ya kuwanyanyua
wakulima nchini,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi huyo wa
TADB aliongeza kuwa Benki yake imejipanga kusaidia mfumo wa Stakabadhi ya
maghala ili kuhakikisha kuwa malengo ya mavuno ya korosho kwa msimu huu
yanafikiwa.
“TADB iko tayari
kuratibu mfumo wa malipo ya fedha zitokanazo na mauzo ya korosho kwa njia ya
TEHAMA, pia kwa kushiriakiana na soko la mazao (TMX), kusimamia ununuzi wa
mazao kwa njia ya mtandao (electronic auction),” aliongeza
Aliongeza kuwa Benki ipo
tayari kusimamia uuzaji wa mazao kwa mifumo ya salama ya kimataifa ya malipo
kama vile dhamana ya malipo.
Naye Mkurugenzi wa
Biashara wa Mikopo wa TADB, Bw. Augustino Chacha alisema kuwa Benki ya Kilimo
ipo tayari kutoa mikopo kwa ajili ya uendelezaji wa miundombinu ya umwagiliaji
na maghala na uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya korosho na mihogo.
Aliongeza kuwa TADB pia
ipo tayari kuviwezesha viwanda vya kubangua mazao ya korosho, na
kusindika ufuta, mihogo pamoja na uanzishaji wa mashamba mapya na ya kisasa ya
korosho na ufuta.
“Tupo tayari kutoa
mikopo kwa ajili ya kuwanyanyua wakulima kama ilivyolengwa na Serikali kupitia
mikopo ya pembejeo kuongeza tija kwenye uzalishaji, miundo mbinu ya umwagiliaji
na ununuzi wa zana za kilimo (kama matrekta, pump),” alisema.
Chacha aliongeza
kuwa kwa kutambua umuhimu wa uhifadhi wa mazao ya kilimo, Benki ya Kilimo ipo
tayari kutoa mikopo kwa ajili ya kujenga maghala mapya au kuboresha yaliyopo
pamoja na kununua mizani ya kisasa na ununuzi wa magari ya usafirishaji mazao.
Akizungumzia nafasi ya
taasisi za kifedha katika kudhibiti upotevu wa mapato kwa wakulima, Mkuu wa
Kilimo na Fedha Vijijini wa Mfuko wa Kukuza Sekta ya Fedha (FSDT), Bw. Mwombeki
Baregu alisema taasisi na mitandao ya simu nchini zina wajibu wa kubuni
teknolojia rafiki wa wakulima itakayosaidia kudhibiti utapeli na wizi wa fedha
za wakulima.
Baregu alisema
teknolojia duni na ukosefu wa elimu sahihi juu ya matumizi na uhifadhi wa fedha
umepelekea wakulima wengi nchini kupoteza mapato yao kwa kushindwa kufahamu
uwekezaji sahihi wa fedha hizo.
“Naziomba taasisi za
kifedha na mitandao ya simu za mkononi kuwasaidia wakulima katika kuhifadhi
fedha zao ili kujiwekea akiba itakayowasaidia wakati wa maandalizi ya kilimo
kwa msimu ujao na shughuli nyingine za kimaendeleo,” alisema.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)
wametakiwa kuongeza jitahada za kuwasajili wanachama wengi wa mfuko huo ili
vituo vya serikali viweze kutoa huduma kwa wananchi wengi
Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki na
Waziri wa Afya,maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto ummy mwalimu wakati
alipotembelea kituo cha afya cha Mazwi kilichopo katika Manispaa ya Wilaya ya
Sumbawanga mwishoni.
Alisema Mkoa wa Rukwa umefikia asilimia
27 ya wananchi wanaotumia bima ya afya Kitaifa,hivyo waongeze kuwashawishi
wananchi wengi zaidi kujiunga na mfuko huo pamoja na mfuko wa afya ya
jamii(CHF)
“nimesema kuanzia sasa ninaanza kuwapima
kwa kusajili wananchi ambao hawapo kwenye mfumo rasmi wa ajira,ninataka vijana
wengi wajiunge kwa wingi kwa kwa kujiunga kama kikundi na kujiunga na bima
inayojulikana kama ‘Kikoa” kwa kujiunga
kikundi cha kuanzia watu kumi,wafikieni huko huko walipo
Kwa upande wa Mfuko wa Afya ya
jamii(CHF) waziri huyo hivi sasa kuna CHF iliyoboreshwa hivyo kadi hiyo
inatumika kwenye vituo vyote vya halmashauri na si pale mwanachama alipokatia,”ni bora
tuwachangishe elfu kumi kumi za watanzania ili tuweze kufikia usajili wananchi
wengi na kupata huduma za afya bila vikwazo
Hata hivyo alishauri Manispaa hiyo
kutengezea kadi ambayo itakua rafiki kwa mwanachama kuweza kuiweka kwenye
waleti au mahali pengine ambayo itakua rahisi kwa kutunza na siyo kadi za hivi
sasa ambayo ni mzigo kwa mwanachama kuibeba kwani kadi hiyo ni kubwa
Pia, alisema wizara yake inataka
kuongeza gharama ya CHF iliyoboreshwa ya shilingi elfu ishirini ambapo mwenye kadi hiyo
ataenda kupata huduma hivyo hadi
hospitali ya mkoa,
“ tunazungumzia kila mtu apate huduma za
tiba bila kikwazo,leo una hela,kesho huna na una umwa bora tunasema utoe elfu
kumi na utibiwe ndani nya manispaa tena siyo peke yako bali na watu wako
watano,alisema waziri ummy.
Hata hivyo alisema ni marufuku
kwa mtu mwenye kadi ya CHF anapoenda kwenye vituo vya huduma ya afya
kuambiwa akanunue kipimo au dawa bali wanatakiwa kupata vipimo vyote.